Wanawake
 wa Vijiji vya Merya na Ikugha katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida 
wameushukuru Mwenge wa Uhuru kwa kuwafungulia mradi ambao umewaepusha 
kutembea umbali mrefu kutafuta maji ya kutumia ambayo si safi wala 
salama huku wakiyachangia na mifugo yao.
Wanawake
 hao wametoa pongezi hizo mara baada ya kiongozi wa mbio za mwenge wa 
uhuru Amour Hamad Amour kufungua mradi wa maji wenye thamani ya zaidi ya
 shilingi milioni 49 utakaohudumia vijiji hivyo ambao umegharimiwa na 
shirika la saving International, halmashauri ya Singida pamoja na 
michango ya wananchi.
Wamesema
 kabla ya kupatikana mradi huo wanawake wa vijiji hivyo wamekuwa 
wakifuata maji umbali mrefu sana kiasi cha kushindwa kutekeleza shughuli
 nyingine za kuzalisha mali.
“Tulikua
 tunatembea mpaka tunachoka, tunaamua kupumzika njiani kwanza ndio 
tuendelee na safari ya kuleta maji nyumbani, yani tunashukuru sana 
kwakweli”, ameongea Bi Greta Senge Mkazi wa kijiji cha Ikugha.
Aidha
 wameongeza kuwa mradi huo utawapatia maji safi na salama kwakuwa maji 
waliyokuwa wakiyafuata umbali mrefu hapo awali yalikuwa machafu na si 
salama.
“Yani
 tulikuwa tunachota maji ambayo unakuta ng’ombe anakunywa hapohapo, 
wakati mwingine anajisaidia na inabidi uchote hivyo hivyo, kwakweli 
tunaushukuru sana mwenge kutufungulia mradi huu, tulikua tunaumwa 
matumbo kila mara”, ameongeza Rehema Lazaro.
Wameongeza
 kuwa mradi huo utapunguza magonjwa ya tumbo na macho ambayo yamekuwa 
yakiwasumbua mara kwa mara hukua wakiridhia kulipia kiasi cha shilingi 
50 kwa lita 20 za maji ili kupata fedha za kutunza mradi huo.
Kwa
 upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Amour Hamad Amour 
ameitaka jumuiya ya watumia maji ya mradi huo kuutunza mradi huo ili 
utoe maji kwa wingi na muda huo kutokanana kuonekana ni hitaji la 
muhimu.
“Nimefika
 hapa na kushuhudia akina mama wengi mnamiminika na ndoo ili mpate maji,
 hii ni ishara kuwa mradi huu ni muhimu hivyo basi jumuiya ya watumia 
maji hakikisheni mda wote maji yanatoka na sio kupanga masaa ya kutoa 
maji au mvua ikinyesha tu mnayafunga, hapana” amesisitiza Amour.
Amesema
 mradi huo usimamiwe vizuri kusiwe na upendeleo au ubaguzi wowote 
kwakuwa maendeleo hayo hayana ubaguzi wa rangi, dini, itikadi za kichama
 au makabila.
Amour
 amesema jumuiya hiyo ihakikishe miundombinu ya mradi huo inatunzwa ili 
kuepusha kuwarudisha akina mama hao katika shida waliyokuwa wakiipata 
awali huku akiwashauri kuangalia namna ya kuipatia mifugo maji pamoja na
 kuweka taratibu nzuri za mapato na matumizi ya mradi huo.
Wakati
 huo huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amezindua mradi wa 
umwagiliaji mbogamboga kwa njia matone wa ekari 25 wenye thamani ya 
shilingi milioni 326 katika kijiji cha Msange.
Akisoma
 taarifa ya mradi huo Afisa Kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Singida 
Adam Mngale amesema mradi huo ulianzishwa mwaka 2012 na hadi sasa una 
wanachama 32 ambao wananufaika kwa kujiongezea kipato kutokana na kulima
 misimu miwili yani kiangazi na masika.
Mngale
 amesema malengo ya mradi huo ni kuongeza eneo la uzalishaji hadi 
kufikia ekari 1400, kupanua miundombinu ili waweze kutumia kutumia bwawa
 la suke na lililoko eneo jirani katika umwagiliaji na kutumia kiwanda 
cha kusindika mbogamboga kilichoko Msange kusindika mazao yao.
0 comments:
Post a Comment