Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mzee
 maarufu na mwenyeji wa Msange Bi Greta Musa Nyonyi akichangia hoja 
katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange 
Wilayani Singida.
 Mratibu
 wa Mradi wa Kupinga Ukeketaji (WOWAP) Nasra Suleiman akizungumza na 
washiriki wa semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya 
Msange Wilayani Singida.
 Afisa
 Maendeleo ya Jamii kata ya Msange Magni Oisso akichangia hoja katika 
semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani 
Singida.
 Washiriki
 wa semina ya kupinga ukeketaji iliyoandaliwa na Mradi wa WOWAP 
wakifuatilia kwa umakini filamu fupi ya Ukeketaji iliyofanyika katika 
Kata ya Msange Wilayani Singida.
Mzee
 wa Kimila Hosea Mnyambi akichangia hoja katika semina ya kupinga 
Ukeketaji iliyofanyika katika Kata ya Msange Wilayani Singida.
Elimu
 sahihi juu ya madhara ya ukeketaji ya muda mfupi na mrefu inatakiwa 
itolewe kwa jamii kabla ya kuwachukulia hatua baadhi yao wanaoendelea 
kufanya vitendo vya ukeketaji licha ya uwepo wa sheria kali.
Rai
 hiyo imetolewa mapema leo na Mratibu wa Mradi wa Kupinga Ukeketaji 
(WOWAP) Nasra Suleiman katika semina ya kupinga Ukeketaji iliyofanyika 
katika Kata ya Msange Wilayani Singida, kwa ushirikiano wa Ofisi ya 
Ustawi wa Jamii Mkoa wa Singida na mradi huo kwa ufadhili wa shirika la 
WAAF-Japan.
Mratibu
 huyo amesema nguvu ya sheria itasaidia kuondoa ukeketaji endapo 
wananchi wengi watakuwa na uelewa wa kutosha juu ya madhara ya ukeketaji
 na kuamua kwa hiyari kuachana na mila hiyo.
“Sheria
 isiwe nguvu pekee ya kupambana na ukeketaji, tukifanya hivyo itafikia 
kipindi tutakwama kwa kiasi kikubwa kwa kuwa watu wataendelea kukeketa 
kwa kificho ili wasikamatwe, lakini kila mwana jamii akiwa na elimu ya 
kutosha ya madhara hayo, nguvu ya sheria itatumika tu kwa wachache watao
 kaidi”, amesisitiza Nasra.
Ameongeza
 kuwa Watendaji wa kata na vijiji wana uwezo mkubwa wa kubadilisha 
mtazamo na mila ya ukeketaji kwa kuelimisha wananchi wao hasa baada ya 
semina zinazoandaliwa na miradi au mashirika Fulani kwakuwa zinawajengea
 uwezo ili waweze kutoa elimu sahihi na mbinu za kuelimisha.
Nasra
 amesisitiza kuwa jukumu la elimu lisiachwe kwa sekta binafsi kama mradi
 wake wa WOWAP pekee bali liwe jukumu la jamii nzima huku akifafanua 
kuwa elimu inayotakiwa kutolewa ni ile inayoelezea madhara ya ukeketaji 
na sio kuwakataza kwa kigezo cha kutii sheria pekee.
Naye
 Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Msange Magni Oisso amesema katika kata
 hiyo ukeketaji umekufanyika kwa siri sana kwa kuogopa mkono wa sheria 
huku wahanga wakiwa watoto wachanga na wale waliomaliza kliniki.
Oisso
 amesema kumekuwa na usiri mkubwa huku wakeketaji wakibadili mbinu namna
 za kujificha wasigundulike kwa jamii ambayo elimu imeanza kuwafikia 
baadhi yao.
Aidha
 amependekeza kuwa ili kukomesha ukeketaji moja ya njia ni kutoa elimu 
katika vituo vya kutolea huduma za uzazi na mtoto ili mtoto aweze 
kunusurika pia elimu itolewe shuleni kwa ngazi zote kuanzia darasa la 
awali hadi la saba.
Akichangia
 mada katika semina hiyo mzee maarufu na mwenyeji wa Msange Bi Greta 
Musa Nyonyi amesema elimu ni bora zaidi kuliko kuwaogopesha wanajamii 
kwa kutumia sheria kwakuwa watatafuta namna ya kutekeleza azma yao kwa 
usiri ili kukwepa mkono wa sheria na sio kuacha.
Greta
 ameongeza kuwa kwa sasa kutokana na kuwa wakeketaji wamebainika kuwa 
wanakeketa watoto wachanga na hugundulika wakienda kliniki baadhi yao 
wanabadili mbinu na kusubiri mtoto amalize kliniki ndipo anakeketwa.
Naye
 Mzee wa Kimila Hosea Mnyambi amesema yeye amekulia katika familia ya 
wakeketaji na wamekuwa wakirithishwa mbinu za ukeketaji kizazi hadi 
kizazi ila kutokana na kuwepo kwa sheria, dini kuhubiri madhara ya 
ukeketaji, mila hiyo wameiacha.
Amesema
 wachache wanaoendelea kufanya vitendo hivy o ha wanawake wamekuwa 
wakifanya kwa usiri mkubwa huku akina baba wakiwa hawana taarifa ya 
kinachoendelea na endapo mtoto anafariki hudanganywa ugonjwa uliopelekea
 kifo cha mtoto.
Mzee
 Mnyambi amesema elimu iendelee kutolewa hasa kwa kutumia vyombo 
vinavyoaminika mfano vyama vya siasa, dini na vikundi vya kuweka na 
kukopa pamoja na kuiweka agenda ya ukeketaji kwa vikao vya Kata na 
vijiji.


0 comments:
Post a Comment