Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu wa Chama Cha Mpira wa miguu wilaya ya Manyoni (MADIFA) Joshua Msemakweli (wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa viongozi wa timu pamoja na wachezaji wa timu zilizoshiriki mchezo wa fainali katika kata ya Sanjaranda. 
MASHINDANO
 ya ligi ya kombe la Diwani wa kata Saranda, Tarafa ya Kilimatinde, 
wilayani Manyoni, Mkoani Singida yamefikia tamati kwa timu ya soka ya 
ILALOO FC kuwa mabingwa wa kombe hilo kwa mwaka huu wa 2017 baada ya 
kuifunga timu ya Saranda FC kwa jumla ya magoli 2-1.
Ligi
 hiyo iliyoanza kuchezwa juni, 29 mwaka huu kwa makundi mawili 
yaliyokuwa yakivitumia viwanja vya michezo vya Shirika la reli Tanzania 
(TRC) ilizishirikisha jumla ya timu sita za kata hiyo ambazo ni pamoja 
na Saranda FC, Ilaloo FC, Irucha, Mlimani A, Mlimani B na Mhegahega FC.
Akitangaza
 matokeo ya mashindano hayo, Katibu wa Chama Cha mpira wa miguu wilaya 
ya Manyoni (MADIFA), Joshua Msemakweli aliwataka vijana hao kuwekeza 
kwenye mchezo wa soka kwa kuamini kwamba michezo ni afya na michezo ni 
ajira.  
“Mashindano
 ngazi ta kata ya Saranda yalishirikisha timu sita kutoka katika vijiji 
na vitongoji,ambavyo ni Kijiji cha Saranda ambapo ndipo makao makuu ya 
kata  pia Ilaloo na Irucha zipo Kijiji cha Saranda Kijiji cha Saranda 
kilikuwa na timu tatu”alifafanua Msemakweli.
Kwa
 upande wake muandaaji wa kombe hilo ambaye pia ni diwani wa kata ya 
Saranda,Joseph Ndahani aliyataja baadhi ya malengo ya michezo hiyo kuwa 
ni kuhakikisha wanakuza pamoja na kuvitangaza vipaji wa vijana wa kata 
hiyo kupitia sekta ya michezo.
Naye
 Mwalimu wa timu ya soka ya Ilaloo FC ambao ndiyo mabingwa wa kombe 
hilo, Rashid Juma alikishukuru kituo hiki kwa kuweza kufika katika Kata 
hiyo na kuwawezesha kusikika maana haijawahi kutokea bahati kama hiyo 
kwa vituo vingine kufika huko. 
0 comments:
Post a Comment