Serikali
 imedhamiria kuwaunganisha wakulima wakubwa wa mazao ya chakula wa kata 
tano za Wilaya ya Iramba kwa kujenga daraja na makaravati manne katika 
barabara yenye urefu wa kilomita 38.6 yatakayo gharimu shilingi bilioni 
4.1.
Akiweka
 jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Mto Mtoa na makaravati katika 
barabara ya shelui-Mtoa-Urughu Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Amour
 Hamad Amour amesema serikali imedhamiria kuwaunganisha wananchi ili 
wazalishe mazao, waanzishe viwanda kisha kusafirisha bidhaa.
Amour amesema kwakuwa barabara hiyo inahudumia wananchi wa  kata
 za Shelui, Mtoa, Mtekente, Urughu na Ndago wananchi wa maeneo hayo 
watumie fursa ya kuwa na barabara nzuri kwa kutengeneza viwanda vidogo, 
vya kati na vikubwa na kisha kusafirisha bidhaa na sio mazao kama mali 
ghafi. 
Amesema
 kwa kufanya hivyo wakulima wa mazao wataweza kujiongeza kipato chao kwa
 kuwa hawatapunjwa kwa kuuzwa mali ghafi ambayo hupelekwa kwenye viwanda
 vya nchi nyingine hivyo barabara hiyo iwe hamasa kwao kuzalisha kwa 
wingi pamoja na kuanzisha viwanda  kwa wingi.
Mradi
 huo wa barabara na makaravati unatekelezwa kupitia mpango wa kuondoa 
vikwazo kwenye barabara za vijijini, mpango unaofadhiliwa na serikali ya
 Tanzania kwa kushirkiana na serikali za Uingereza na Ireland Kaskazini.
Kukamilika
 kwa ujenzi wa daraja na makaravati hayo kutawezesha barabara hiyo 
kupitika kwa kipindi cha mwaka mzima na hivyo kuwanufaisha wakazi elfu 
79 wa kata hizo pamoja na kuwezesha utoaji wa huduma za kijamii katika 
eneo hilo lenye shule za msingi 29, shule za sekondari 6, zahanati 7 na 
kituo cha afya kimoja.
Wakati
 huo huo Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Amour Hamad Amour amezindua
 mradi wa ghala la kuhifadhia chakula katika kijiji cha Nselembwe ambalo
 litakuwa likihudumia jamii ya kata za Ulemo,Mgongo, Ntwike, Shelui na 
Mtoa.
Akifungua
 ghala hilo Amour amesema kauli mbiu ya mwenge wa uhuru mwaka huu ni 
shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya taifa hivyo ujenzi wa 
ghala ili kuhifadhi mazao unasaidia wananchi kutoyauza ovyo mazao na 
kuyahifadhi mahali salama kabla ya kuyachakata kuwa bidhaa.
Amesema
 mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 350 utaweza kuwasaidia 
wananchi kuhifadhi mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani na kuwa na 
kauli moja juu ya bei ya mazao pia watakua na uhakika wa mazao.
Amour
 amewasisitiza wananchi wa kata hizo kuzalisha kwa wingi kwa kuwa sasa 
wana uhakika wa sehemu salama ya kutunzia mazao yao ili wasishawishike 
kuyauza kwa bei ndogo.
Mwenge
 wa Uhuru ukiwa Wilayani Iramba umetembelea miradi yenye thamani ya 
shilingi bilioni 4.8 huku ukipitia miradi 6 na kuona shughuli 5 katika 
vijiji  10 na tarafa 4 katika umbali wa km 119.1.

0 comments:
Post a Comment