Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu
 wa Mkoa wa Singia Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na Meya wa Manispaa ya
 Singida Gwae Chima Mbua kabla ya kuanza kwa baraza Maalumu la madiwani 
wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
 Mkurugenzi
 wa Manispaa ya Singida Bravo Kizito Lyampembile akifungua baraza 
Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa 
Fedha za Serikali.
 Baadhi
 ya Viongozi wa Manispaa ya Singida wakifuatilia baraza Maalumu la 
madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za 
Serikali.
 
 Madiwani wa manispaa ya Singida wakifuatilia baraza Maalumu la madiwani
 wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa Fedha za Serikali.
Madiwani
 wa manispaa ya Singida wakiwa wamesimama kuridhia hoja katika baraza 
Maalumu la madiwani wa Manispaa ya Singida kujadili hoja za Mkaguzi wa 
Fedha za Serikali.
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amesema hatavumilia kuona 
halmashauri inafanya uzembe na kupata hati chafu ya Mkaguzi na Mdhibiti 
wa Fedha za Serikali kwakuwa itamchafua yeye na taswira ya uongozi wote 
wa Mkoa wa Singida.
Dkt
 Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema jana wakati wa baraza maalumu la 
madiwani wa Manispaa ya Singida la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti 
wa Hesabu za serikali ambazo amesema hoja nyingi zimetokana na uzembe.
Amesema
 licha ya kuipongeza Manispaa ya Singida kwa kupata hati safi, uwepo wa 
hoja umedhihirisha kuwa kuna baadhi ya watendaji wanafanya kazi kwa 
uzembe na kutofuata taratibu na sheria hivyo wajirekebishe haraka.
Dkt
 Nchimbi ameongeza kuwa hoja nyingi zinajitokeza kwa kukosa umakini na 
watendaji kufanya kazi kwa mazoea hali ambayo ikiendelea inaweza 
kuipelekea manispaa kupata hati isiyoridhisha hivyo kupata hati safi 
kuwaongezee nguzu ya kuboresha utendaji kazi wao.
Aidha
 amewashauri wakuu wa idara na watumishi wengine kuitendea haki manispaa
 yao kwa kuchapa kazi kuwa wadilifu na kufuata sheria kwani wakifanya 
hivyo wataepuka hoja zisizo za lazima na kuharakisha maendeleo.
Dkt
 Nchimbi amewasisitizia matumizi ya muda kuwa yenye tija ambapo amelaani
 kitendo cha kutumia muda mwingi kwenye vikao ambavyo havina tija bali 
watumie muda kidogo kwenye vikao na muda mwingi kutatua kero za 
wananchi, huku akiahidi kufuatilia matumizi ya muda unaotumika kwenye 
vikao.
Ameongeza
 kuwa watendaji wote wanapaswa kubadilika na kuendana na kasi ya Rais wa
 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Hapa kazi tu ili waweze kupunguza 
hoja na kufuta zile zisizo za lazima.
Kwa
 upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina Lutambi amewaasa
 watendaji kuitumia vema dhamana ya utumishi wa umma kwa kuhakikisha 
wanaleta mabadiliko ya kimaendeleo.
Dkt
 Lutambi ameongeza kuwa watumishi wa umma wanapaswa kufahamu kuwa 
jutendaji wao ukilega lega athari yake inamkumba mwananchi kwakuwa 
atachelewa kupata maendeleo, hivyo bidii katika utumishi umma ni muhimu.
Amewasisitizia
 kuwa mikakati na malengo ya maendeleo ya kimkoa na kitaifa haitaweza 
kufikia endapo watendaji hawatakuwa waadilifu na wakiendekeza uzembe 
hivyo wajitume kwa bidii kwa manufaa ya taifa kwa ujumla.
Naye
 Diwani Viti maalumu Magreth Malecela amemshukuru Mkuu wa Mkoa Dkt 
Nchimbi kwa kuwapa vyeti ambavyo vilitolewa kwa madiwani wote waliopata 
mafunzo ya usimamizi wa ruzuku na miradi ya serikali.
Malecela
 ameongeza kuwa ushirikiano na ushauri wanoaupata kutoka kwa Dkt Nchimbi
 utaisaidia manispaa kuwa na maendeleo huku akiahidi kwa niaba ya 
madiwani wenzake kuwa watafuata maelekezo na ushauri kwa manufaa ya 
manispaa ya Singida.
 

0 comments:
Post a Comment