Katibu
 Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji 
akisoma bango mara baaa ya kuzindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana 
na shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida.
Mkurugenzi wa Shirika la AMDT Michael Kayombo akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.
 Baadhi
 ya wadau waliohudhuruia uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la 
kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.
 Mkurugenzi
 wa mradi wa Faida Mali mkoa wa Singida Tom Silayo akisoma taarifa ya 
mradi huo kwa wajumbe waliohudhuria uzinduzi wa mradi utakaowasaidia 
wakulima kulima alizeti kibiashara.
 Mtendaji
 Mkuu wa Chama cha wasindikaji wa Mbegu za alizeti Tanzania Daud Musa 
Mwasantaja akiwahakikishia wakulima wa alizeti upatikanaji wa soko 
katika uzinduzi wa Mradi wa Faida Mali.
Wauzaji
 wa pembejeo ambao sio waaminifu wamepewa onyo kali na endapo atabainika
 yeyote anayewalaghai wakulima na kuwauzia pembejeo ambazo sio hali 
hatua kali dhidi yake zitachukuliwa.
Katibu
 Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji 
ametoa onyo hilo wakati akizindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana na 
shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa alizeti Mkoani Singida ili
 kulima zao hilo kibiashara zaidi.
Chowaji
 amesema kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya wakulima ambao hukumbana
 na wauzaji wa pembejeo ambao sio waaminifu na kuwalaghai kwakuwa 
wakulima hao hawana elimu na uelewa hasa wa viuatilifu au mbegu ambazo 
ni halisi.
Ameongeza
 kuwa mkono wa serikali ni merfu na utawabaini popote walipo hivyo 
waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo wanakirudisha nyuma kilimo cha 
alizeti ambacho ni tegemeo kwa ajili ya uchumi wa viwanda Mkoani 
Singida.
“Singida
 tuna Viwanda vya kuamua mafuta ya alizeti vikubwa viwili, vya kati 
vitatu na vidogo 115 na kufanya jumla ya viwanda vya alizeti kuwa 120, 
vyote hivyo vinategemea alizeti ya mkulima, lakini pia mkulima anakuwa 
na matarajioa makubwa, hao wauzaji pembejeo wasio waaminifu 
hatutawavumilia, tena waache mara moja”, amesisitiza Chowaji.
Aidha
 amelipongeza shirika la AMDT kupitia mradi wa Faida mali kwa kuuchagua 
Mkoa wa Singida ili kuboresha kilimo cha alizeti hasa kwa ajili ya 
mkulima mdogo.
Chowaji
 amesema viwanda vya alizeti Mkoani Singida hufanya kazi kwa miezi 
minane kwa mwaka badala ya mwaka mzima kutokana na kuwa alizeti 
inayozalisha bado haitosheleshi viwanda hivyo kufanya kazi mwaka mzima.
Amesema
 matumaini makubwa ya serikali mkoani hapa ni kuwa mradi huo utasaidia 
kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili kuifanya Singida ya Viwanda kuwa 
bora zaidi pamoja na kuliboresha zao lenyewe la alizeti kwa kutumia 
pembejeo za kisasa zaidi.
Chowaji
 amewataka wakulima wote wa alizeti kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiunga
 katika vikundi ili waweze kufikiwa kwa urahisi na kunufaika, pia waache
 kilimo cha mazoea kwakuwa alizeti ni biashara kubwa ambayo itawakomboa 
kiuchumi na kukupa pato la mkoa wa Singida.
Kwa
 upande wake Mkurugenzi wa Shirika la AMDT Michael Kayombo amesema 
shirika hilo kupitia Mradi wa Faida mali utahakikisha unasaidia 
upatikanaji wa mikopo kwa wakulima wadogo wa alizeti Mkoani singida.
Kayombo
 ameongeza kuwa mradi utaboresha huduma za ugani kwa kutoa taarifa 
sahihi na mapema juu ya kilimo cha alizeti kwa wakulima na taarifa hizo 
zitatolewa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno hivyo kuwafikia mapema.
Amreongeza
 kuwa watahakikisha wakulima wanapata soko la uhakika la zao hilo ndani 
na nje ya mkoa wa singida pamoja na kuhakikisha bei ya zao hilo ni yenye
 kumnufaisha mkulima na sio kumdidimiza zaidi.
Naye
 Mtendaji Mkuu wa Chama cha wasindikaji wa Mbegu za alizeti Tanzania 
Daud Musa Mwasantaja amesema viwanda vya alizeti bado vina uhitaji 
mkubwa wa alizeti kwa kuwa viwanda vyao vimekuwa vikiendeshwa chini ya 
malengo kutokana na mbegu hizo kuwa chache.
Mwasantaja
 amesema wana imani kuwa mraadi wa Faida Mali utasaidia kuongeza 
uzalishaji wa alizeti hivyo kuwasaidia kuongeza pia uzalishaji katika 
viwanda vyao.
Ameongeza
 kuwa watatoa ushirikiano wa kutosha na hivyo wakulima wasiwe na 
wasiwasi walime zao hilo kwa wingi watapata wateja na kwa bei ambayo ni 
nzuri.
Nao
 wakulima walioshiriki uzinduzi wa maradi huo wamesema mradi huo umekuja
 muda muafaka kwakuwa na wao wanatamani kupata faida kutokana na kilimo 
hicho kwakuwa baadhi bado wanalima kwa mazoea na kwa kutumia mbegu 
ambazo hazizalishi kwa wingi.
0 comments:
Post a Comment