Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu
 wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akipiga saluti wakati wa 
paredi ya polisi iliyoandaliwa lililoandaliwa  kwa ajili yake kulikagua 
mapema leo kwenye viwanja vya kambi ya  FFU mjini hapa.
Mkuu
 wa Jeshi la Polisi  nchini IGP Simon Sirro akikagua baadhi ya askari wa
 jeshi la polisi  mjini  Singida leo piga saluti wakati wa paredi ya 
polisi iliyoandaliwa lililoandaliwa  kwa ajili yake kulikagua.
Mkuu
 wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro akizungumza na waandishi wa 
habari muda mfupi baada kukagua askari polisi waliokuwa kwenye  paredi 
kwenye viwanja vya kambi ya  FFU mjini hapa.
………………………….
Picha/Habari na Gasper Andrew.
Mkuu
 wa Jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro amelipongeza jeshi la 
polisi Mkoani Singida kwa juhudi zake za kupunguza matukio ya uhalifu 
yakiwemo ya utekeji wa magari kwa kiwango kikumbwa.
IGP 
 Siro ametoa pongezi hizo  leo asubuhi alipokuwa akizungumza na 
waandishi wa habari  kweye viwanja vya kambi  ya kikosi  cha kuzuia fujo
 (FFU) mjini  hapa.
Amesema matukio
 ya uhalifu mbalimbali mkoani Singida yamekupungua kwa kiwango kikubwa 
kwa  sasa, ikilinganishwa na miaka ya  nyuma.
“Hatua
 hii  inachangia  uwepo  wa amani  na utulivu kwa  wananchi  wa  mkoa wa
 Singida hivyo  kutoa fursa   kuweza  kujiletea maendeleo yao ya mkoa 
na  taifa   kwa ujumla” amesema.
IGP
 Siro  amesema  mafanikio  hayo yamechangiwa   na wananchi kwa kiwanngo 
 kikubwa  kwa kutoa ushuirikiano  kwa jeshi la polisi. 
Akifafanua
 amesema wananchi wamekuwa wakitoa  taarifa sahihi na kwa  wakati kwa 
jeshi la polisi  pindi wanapobaini  dalili  ama  matukio ya kihalifu.
“Kwa
 sasa kwa kweli  wananchi hata ninyi waandishi  wa habari mnatupa  
ushirikiano  mzuri sana. Ushirikiano huu unachangia  kazi zetu kuwa 
nyepesi  na za mafanikio makubwa. Sasa  hivi  kule Kibiti mkoani Pwani, 
wananchi wanatusaidia mno taarifa  zinazohusu  mauaji ya watu  
wasiokuwa  na hatia”, amefafanua zaidi.
IGP
 Siro amesema kwa sasa Tanzania inaonewa wivu na nchi jirani kwa namna 
tulivyo dhibiti matukio ya kihalifu na kupelekea nchi kuendelea 
kudumisha amani na utulivu.
Wakati
 huo huo, Mkuu huyo  wa jeshi la polisi ametumia fursa hiyo  kuwaomba 
wananchi  waendelee  kushirikiana na jeshi hilo, kufichua  baadhi ya 
watu wanaojihusisha na matukio mbalimbali   ya kihalifu ili waweze 
kuchukulia  hatua stahiki.
0 comments:
Post a Comment