Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
29 January 2018
MADIWANI na Watumishi wa wa Manispaa ya Tabora wameagizwa kufuatilia makusanyo ya katika  Stendi za Mabasi ya Tabora ili kujua mapato halisi yanayopatikana kila siku kwa ajili  kudhibiti upotevu wa makusanyo katika stendi hiyo na kuiongezea Halmashauri hiyo makusanyo yake ya ndani.
Kauli
 hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Queen Mlozi wakati 
akizungumza na Madiwani na Watumishi wakati wa kikao maalum cha kujadili
 rasmi ya mpango wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha.
Alisema
 kuwa ni vema watembelea Stendi hiyo na kuangalia utaratibu unatumika 
katika ukusanyaji mapato kutokana na magari yanapita na yale stendi hiyo
 ili kujua fedha taslimu zinapatikana na kwa mwaka jambo 
litakalowawezesha kujua Halmashauri inatakiwa ipate kiasi gani.
“Waheshimiwa
 Madiwani nawaombeni sana muangalie upya makusanyo katika vyanzo vyenu 
mbalimbali kama vile stendi na matangazo ili kujiridhisha kama 
Halmashauri inachopata kinalingana na hali halisi au kuna mianya ya 
upotevu ili tuizibe mapema” alisema Mkuu huyo wa Wilaya.
Alisema
 kuwa hatua itawasaidia kutekeleza maelekezo ya viongozi ikiwemo yale ya
 Waziri Mkuu ya kutaka kila Halmashauri kuhakikisha inakusanya sio chini
 ya 80 ya mapato yake ya ndani kila mwaka nje ya hapo viongozi 
watawajibishwa.
Queen
 aliongeza kuwa haipendezi kwa Halmashauri kama Tabora kujieleza kwa 
kushindwa kufikia lengo wakati inaweza kubuni vyanzo mbalimbali ambavyo 
vitawasaidia kuvuka lengo.
Alisema kuwa wanaweza kuanzisha eneo maaalumu kwa ajili ya  wafanyabiashara (Machinga) kila mara moja kwa wiki ambalo linaweza kuwa chanzo kingine cha mapato.
Naye
 Diwani wa Kata ya Ng’ambo George Mpepo aliwaomba Madiwani wenzake 
kuufanyia kazi ushauri wa Mkuu huyo wa Wilaya kwa sababu utawasaidia 
kuongeza makusanyo na kuwa na fedha kwa ajili ya kuwaletea maendeleo 
wakazi wa Manisapaa ya Tabora.
Alisema
 kuwa haipendezi kuona Halmashauri nyingine zinavuka lengo huko kila 
mwaka inashindwa na kuongeza kuwa wakiendelea kushindwa ni vema Baraza 
hilo la Madiwani livunjwe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.
“Mheshimiwa
 Mkuu wa Wilaya ushauri wako umenigusa sana…naomba wenzangu 
tukayazingatie hayo…na kama tutashindwa nitakuomba umuombe Waziri Mkuu 
avunje Baraza hilo la Madiwani kwa kushindwa kusimamia shughuli 
mbalimbali za maendeleo kuifanya Manispaa ya Tabora iendelee kuwa nyuma”
 alisema Mpepo.
Mwisho

0 comments:
Post a Comment