Mkuu
 wa Mkoa wa Singida, Dk. Rehema Nchimbi, ameonya kuwa watu watakaovuruga
 mikutano ya kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Singida 
Kaskazini, serikali itawashughulikia kwa mujibu wa sheria.
Dk.
 Nchimbi alitoa onyo hilo katika Kijiji cha Mtinko Wilaya ya Singida 
Vijijini alipokuwa akitoa taarifa ya mafanikio ya serikali ya awamu ya 
tano kwenye uzinduzi wa kampeni hizo.
Alisisitiza
 kwamba ili watambue kuwa ni mtumishi aliyetumwa na Chama Cha Mapinduzi 
(CCM), ajitokeze mtu yeyote na kuthubutu kuvuruga ratiba ya mikutano ya 
kampeni.
Hata
 hivyo, aliwahakikishia wananchi kuwa mikutano ya kampeni itakuwa salama
 pamoja na uchaguzi huo kwani serikali imejipanga kikamilifu kudhibiti 
yeyote atakayeonekana anataka kuvuruga uchaguzi huo.
“Na
 ole wake na atokee mtu yeyote yule mwingine atakaeingilia katika njia 
hii ya uchaguzi salama, amani na utulivu ndipo mtakapotambua kwamba 
nimetumwa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi,” alisema na kuongeza:
“Jiandaeni vizuri na wakati wa kura mjitokeze kwa wingi kupiga kura na kumchagua mgombea wa CCM, na siyo mwingine.”
Dk.Nchimbi
 aliyataja baadhi ya mafanikio yaliyopo katika jimbo hilo ni bomba na 
mafuta kutoka Horiri Uganda hadi Tanga ambalo kwa Singida Kaskazini lina
 sifa ya pekee yake na litakuwa limenyanyuka kiuchumi kuliko sehemu 
yeyote litakapopita.
“Na
 hapa Singida Kaskazini kutajengwa kambi, patajengwa kituo watakuja 
wataalamu na mabingwa wa hilo bomba ambao watakaa hapa kwa zaidi ya 
miaka mia moja, hawatakaa pengine bali watakuja kukaa Singida 
Kaskazini,”alisema.

0 comments:
Post a Comment