Singida kujenga machinjio ya kuku wa asili

WILAYA ya Iramba mkoani Singida inatarajia kuanzisha machinjio ya kuku wa asili ifikapo Julai mwakani. Mkuu wa wilaya  hiyo bwana Yahaya Nawanda amebainisha hayo Mjini Kiomboi wakati akifungua   mafunzo ya siku mbili juu ya ufugaji kuku kisasa na kuanzisha SACCOS ya  wafugaji kuku Amesema lengo la machinjio hayo ya kisasa yaliyopangwa kujengwa katika mji wa Misigiri ni kuhakikisha  kuwa kuku wanaozalishwa wanaongezwa thamani kwa kuchinjwa na kusindikwa ili kukidhi mahitaji ya soko badala ya kusafirishwa hai kwa adha kubwa na wengine kufa njiani. Amesema uamuzi  wa kujenga machinjio  hayo  umefikiwa baada ya kubaini kuwa licha ya ufugaji wa kuku wa asili kuwa moja ya shughuli kuu za kiuchumi mkoani  Singida, kumekuwepo na changamoto mbalimbali. Amesema...

Bilioni 6.4 zatumika ujenzi wa barabara Singida

ZAIDI  ya shilingi  bilioni 6.4 zimetumika kwa ajili ya shughuli  za  matengenezo ya barabara kuu, mkoa na madaraja  katika mkoa wa  Singida katika kipindi cha kuanzia  Januari hadi  Juni mwaka huu.. Kaimu meneja wa wakala wa baraara TANROADS mkoa wa Singida Mhandisi Yohannes Mbegalo, amebainisha hayo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha 35 cha bodi ya barabara. Mhanadisi  Mbegalo amesema  kuwa  fedha hizo zimetumika  kwa  ajili ya kugharamia  shughuli  za matengenezo ya kawaida kwa upande wa barabara za lami na changarawe zilizopo  mkoani Singida. Amebainisha baadhi ya shughuli zilizofanyika kuwa ni pamoja na  matengenezo ya sehemu korofi, matengenezo ya vipindi maalum pamoja na matengenezo...

Wanafunzi wabuni kifaa cha kumwagilia

Wanafunzi wawili Fideli Samwel na Jafari Ndagula kutoka shule ya sekondari Ilongero, iliyopo mkoani Singida, wameibuka washindi katika mashindano ya sayansi kwa vitendo iliyoshirikisha mikoa 18 nchini. Mashindano hayo yalishirikisha wanafunzi 120 kutoka  shule za sekondari 60 pamoja na walimu wao wa sayansi, kwa ajili ya kuonyesha ubunifu na vipaji vya kisayansi ili kuzalisha wataalamu wengi nchini. Ndagula alizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki baada ya kutangazwa kuwa mshindi, alisema kubuni kifaa cha umwagiliaji, hawakuwa na uhakika wa kushinda kwenye maonyesho hayo na kwamba wanamshukuru Mungu kuwafanikisha. Kifaa hicho kinatumika kama pampu ya kusukuma maji ambayo ina mipira maalumu inayoweza kumwagilia shamba au bustani. “Unajua mashindano yalikuwa...

Hii Hatari :Vyandarua vyatumika kuezeka vyoo badala ya kukinga Mbu!

  Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida Edward Ole Lenga akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa Zahanati na nyumba mbili za mganga na shirika moja lisilo la kiserikali la HAPA,hafla hiyo ilifanyikajuzi kijijini hapo.  Ni Mwakilishi wa shirika la SIMAVI kutoka nchini Uholanzi Lieke Ongering akizungumza katika hafla ya kukabidhi mradi wake kwa ushirikiano na shirika la HAPA Singida kukamilisha mradi wa ujenzi wa Zahanati na nyumba mbili za mganga kijiji cha Kinampundu takribani umbali wa kilomita 70 kutoka mjini Singida. Ni mmoja...

WFP watoa msaada wa pampu za maji zenye thamani Tsh 94 millioni mkoani Singida

Mkuu wa Ofisi ndogo ya Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dodoma, Nima Sitta akihimiza utunzaji wa matenki ya kuvunia maji ya mvua yaliyojengwa katika shule za msingi wilaya ya Singida na Ikungi. Shirika la WFP limetoa shilingi 95,271,600 kugharamia ujenzi wa matenki hayo.(Picha  na Nathaniel Limu). Na Nathaniel Limu Shirika lisilo la kiserikali la Mpango wa chakula duniani (WFP) limetoa msaada wa pampu 210 za maji zenye thamani ya zaidi ya shilingi 94 milioni kwa shule za msingi na vikundi mbalimbali mkoani Singida. Pampu hizo ni kwa ajili ya kilimo cha umwangiliaji bustani. Hayo ...

Mkandarasi atishia kujitoa ujenzi wa barabara

KAMPUNI ya China ya Sinohydro imetishia kusimamisha ujenzi wa barabara ya lami ya Manyoni- Itigi mkoani Singida hadi Chaya mpakani mwa Tabora kutokana na kuidai Serikali zaidi ya Sh bilioni 14.7. Madai hayo ni sehemu ya gharama za ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 89.3 kwa kazi ambayo imekwishafanyika. Hali hiyo inatajwa kuwa moja ya sababu za utekelezaji wa mradi huo kuwa nyuma kwa zaidi ya miezi sita sasa kutokana na mkandarasi kukabiliwa na uhaba wa fedha. Mkandarasi mshauri wa mradi huo Nicholas Geyer kutoka Ireland, alisema kutokana na madai ya fedha kwa muda mrefu bila mafanikio, shughuli hiyo inaweza kusimamishwa wakati wowote. Alisema hatua hiyo itakachelewesha zaidi ujenzi na kuigharimu Serikali kwa kulazimika kulipa fidia kwa mujibu wa sheria za mikataba. Hata...

Halmashauri ya Singida yakusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 22 kutoka vyanzo yake mbalimbali.

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida Jumanne Mnyampanda (katikati) akiongoza kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wanancvhi mjini Singida. Wa kwanza kushoto ni makamu mwenyekiti halmashauri ya wilaya ya Singida Hamisi Mumbee na kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Singida Illuminata Mwenda.  Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Singida wakifuatilia kwa makini hoja zilizokuwa zikijadiliwa kwenye kikao cha baraza la madiwani. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini Singida. Mwenyekiti ...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa