WILAYA ya Iramba mkoani Singida
inatarajia kuanzisha machinjio ya kuku wa asili ifikapo Julai mwakani.
Mkuu wa wilaya hiyo bwana Yahaya Nawanda
amebainisha hayo Mjini Kiomboi wakati akifungua mafunzo ya siku
mbili juu ya ufugaji kuku kisasa na kuanzisha SACCOS ya wafugaji kuku
Amesema lengo la machinjio hayo ya kisasa
yaliyopangwa kujengwa katika mji wa Misigiri ni kuhakikisha kuwa kuku
wanaozalishwa wanaongezwa thamani kwa kuchinjwa na kusindikwa ili kukidhi
mahitaji ya soko badala ya kusafirishwa hai kwa adha kubwa na wengine kufa
njiani.
Amesema uamuzi wa kujenga machinjio
hayo umefikiwa baada ya kubaini kuwa licha ya ufugaji wa kuku wa asili
kuwa moja ya shughuli kuu za kiuchumi mkoani Singida, kumekuwepo na
changamoto mbalimbali.
Amesema...
Bilioni 6.4 zatumika ujenzi wa barabara Singida
ZAIDI ya
shilingi bilioni 6.4 zimetumika kwa ajili ya shughuli za
matengenezo ya barabara kuu, mkoa na madaraja katika mkoa wa
Singida katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Juni mwaka
huu..
Kaimu
meneja wa wakala wa baraara TANROADS mkoa wa Singida Mhandisi Yohannes Mbegalo,
amebainisha hayo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha 35 cha bodi ya
barabara.
Mhanadisi
Mbegalo amesema kuwa fedha hizo zimetumika kwa ajili ya
kugharamia shughuli za matengenezo ya kawaida kwa upande wa
barabara za lami na changarawe zilizopo mkoani Singida.
Amebainisha baadhi ya
shughuli zilizofanyika kuwa ni pamoja na matengenezo ya sehemu korofi,
matengenezo ya vipindi maalum pamoja na matengenezo...
Wanafunzi wabuni kifaa cha kumwagilia
Wanafunzi wawili Fideli Samwel na Jafari Ndagula kutoka
shule ya sekondari Ilongero, iliyopo mkoani Singida, wameibuka washindi katika
mashindano ya sayansi kwa vitendo iliyoshirikisha mikoa 18 nchini.
Mashindano hayo yalishirikisha wanafunzi 120 kutoka shule za sekondari 60
pamoja na walimu wao wa sayansi, kwa ajili ya kuonyesha ubunifu na vipaji vya
kisayansi ili kuzalisha wataalamu wengi nchini.
Ndagula alizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki baada ya
kutangazwa kuwa mshindi, alisema kubuni kifaa cha umwagiliaji, hawakuwa na uhakika
wa kushinda kwenye maonyesho hayo na kwamba wanamshukuru Mungu kuwafanikisha.
Kifaa hicho kinatumika kama pampu ya kusukuma maji ambayo ina mipira maalumu
inayoweza kumwagilia shamba au bustani.
“Unajua mashindano yalikuwa...
Hii Hatari :Vyandarua vyatumika kuezeka vyoo badala ya kukinga Mbu!
Mkuu
wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida Edward Ole Lenga akizungumza na
wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa Zahanati na
nyumba mbili za mganga na shirika moja lisilo la kiserikali la
HAPA,hafla hiyo ilifanyikajuzi kijijini hapo.
Ni
Mwakilishi wa shirika la SIMAVI kutoka nchini Uholanzi Lieke Ongering
akizungumza katika hafla ya kukabidhi mradi wake kwa ushirikiano na
shirika la HAPA Singida kukamilisha mradi wa ujenzi wa Zahanati na
nyumba mbili za mganga kijiji cha Kinampundu takribani umbali wa
kilomita 70 kutoka mjini Singida.
Ni
mmoja...
WFP watoa msaada wa pampu za maji zenye thamani Tsh 94 millioni mkoani Singida
Mkuu
wa Ofisi ndogo ya Mpango wa Chakula Duniani (WFP) Dodoma, Nima Sitta
akihimiza utunzaji wa matenki ya kuvunia maji ya mvua yaliyojengwa
katika shule za msingi wilaya ya Singida na Ikungi. Shirika la WFP
limetoa shilingi 95,271,600 kugharamia ujenzi wa matenki hayo.(Picha na
Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu
Shirika
lisilo la kiserikali la Mpango wa chakula duniani (WFP) limetoa msaada
wa pampu 210 za maji zenye thamani ya zaidi ya shilingi 94 milioni kwa
shule za msingi na vikundi mbalimbali mkoani Singida.
Pampu hizo ni kwa ajili ya kilimo cha umwangiliaji bustani.
Hayo
...
Mkandarasi atishia kujitoa ujenzi wa barabara
KAMPUNI ya China
ya Sinohydro imetishia kusimamisha ujenzi wa barabara ya lami ya Manyoni- Itigi
mkoani Singida hadi Chaya mpakani mwa Tabora kutokana na kuidai Serikali zaidi
ya Sh bilioni 14.7. Madai hayo ni sehemu ya gharama za ujenzi wa barabara hiyo
yenye urefu wa kilomita 89.3 kwa kazi ambayo imekwishafanyika.
Hali hiyo inatajwa kuwa moja ya sababu za
utekelezaji wa mradi huo kuwa nyuma kwa zaidi ya miezi sita sasa kutokana na
mkandarasi kukabiliwa na uhaba wa fedha.
Mkandarasi mshauri wa mradi huo Nicholas Geyer
kutoka Ireland, alisema kutokana na madai ya fedha kwa muda mrefu bila
mafanikio, shughuli hiyo inaweza kusimamishwa wakati wowote.
Alisema hatua hiyo itakachelewesha zaidi ujenzi
na kuigharimu Serikali kwa kulazimika kulipa fidia kwa mujibu wa sheria za
mikataba.
Hata...
Halmashauri ya Singida yakusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 22 kutoka vyanzo yake mbalimbali.

Mwenyekiti
wa halmashauri ya wilaya ya Singida Jumanne Mnyampanda (katikati)
akiongoza kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa
mikutano wa chuo cha maendeleo ya wanancvhi mjini Singida. Wa kwanza
kushoto ni makamu mwenyekiti halmashauri ya wilaya ya Singida Hamisi
Mumbee na kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Singida Illuminata
Mwenda.
Baadhi
ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Singida wakifuatilia kwa makini
hoja zilizokuwa zikijadiliwa kwenye kikao cha baraza la madiwani. Kikao
hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya
wananchi mjini Singida.
Mwenyekiti
...