Kaimu
 kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP, Thobius Sedoyeka, 
akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya mauaji ya watu wawili 
wakazi wa wilaya ya Ikungi akiwemo mmoja kuuawa kwa kutuhumiwa kuwa na 
mahusiano ya kimapenzi na mama mzazi wa muuaji. Salumu Juma mkazi wa 
kijiji cha Makotea, amemuawa Faraja Emmanuel, kwa madai kuwa ana 
mahusiano ya kimapenzi na mama yake.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MKULIMA
 mmoja na mkazi wa kijiji cha Makotea wilaya ya Ikungi mkoa wa 
Singida,Salumu Juma (37) amefariki dunia baada ya kushambuliwa vibaya na
 Faraja Emmanuel  kwa tuhuma ya kuwa na mahusiano ya mapenzi na mama 
yake.
Kaimu
 Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida,ACP Thobius Sedoyeka amesema 
tukio hilo limetokea aprili 19 mwaka huu saa saba mchana huko katika 
hospitali ya misioni ya Makiungu wilaya ya Ikungi.
Amesema
 siku ya tukio,mtuhumiwa Salumu alimvia njiani Faraja na baada ya 
kumvamia alimshambulia kwa kutumia rungu sehemu mbalimbali za mwili  na 
kisha kumvunja miguu yote miwili.
“Salumu
 baada ya kutimiza azma yake hiyo alimwacha Faraja akiwa amezirai na 
yeye kulimbilia kusikojulikana wasamaria wema waliweza kumwokota Salumu 
na kisha kumkimbiza katika hospitali ya Makiungu ambapo alifariki akiwa 
anaendelea kupatiwa matibabu”,alifafanua zaidi,Sedoyeka.
Amesema
 uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Salumu ametenda kosa hilo baada ya 
kuchukizwa na tabia ya Faraja kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mama 
yake mzazi.
“Kwa sasa tumeanzisha msako mkali wa kumtafuta Salumu ili amweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Katika
 tukio jingine,Sedoyeka amesema kuwa Joram Joseph (36) mkulima na mkazi 
wa kijiji cha Msimii kata ya Sepuka wilaya ya Ikungi,amefariki dunia 
baada ya kuchomwa kisu shingoni na bega la kushoto na baba yake mzazi 
Joseph Benjamin (61).
Amesema tukio hilo limetokea Aprili 21 mwaka huu saa moja usiku huko katika kijiji cha Msimii Sepuka.
Kaimu
 kamanda huyo amesema chanzo cha mauaji hayo ni kutokana na Joram 
kumtukana matusi ya nguoni baba yake mzazi.Joramu inadaiwa kutoa matusi 
hayo kutokana na kulewa pombe ya kienyeji kupindukia.
“Baada ya mauaji hayo,mtuhumiwa mzee Joseph aliweza kujisalimisha mwenye katika kituo cha polisi cha Sepuka”,amesema Sedoyeka.
Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment