Ofisi
 ya Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida imedhamiria kusimamia uboreshaji wa 
huduma za maji mkoani hapa huku mizaha itakayofanywa na mtu yeyote 
katika miradi ya maji, kutovumiliwa. 
Kaimu
 Katibu Tawala Sehemu ya Maji Mkoa wa Singida Mhandisi Lyidia Joseph 
amebainisha hayo leo wakati wa kikao maalumu na Timu ya usimamizi wa 
sekta ya maji ya halmashauri ya Wilaya  ya Manyoni, kwa ajili ya kufuatilia usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maji.
Mhandisi
 Lydia amewaeleza wataalamu hao kuwa uongozi wa mkoa hautavumilia endapo
 kuna mtumishi yeyote atafanya mzaha katika kusimamia miradi ya maji 
kwakuwa mkoa umekuwa ukitoa ushirikiano wa kutosha hivyo hakuna sababu 
ya kushindwa kufanya vizuri.
“Sisi
 katika ngazi ya mkoa hatutavumilia mzaha katika masuala ya maji, tupo 
tayari kutoa ushirikiano popote mnapoona mnakwama ili tu tufikie malengo
 yetu ya kutoa huduma bora za maji kwa wananchi, hali ilivyo sasa 
hairidhishi kabisa, tufanye kazi kwa kasi zaidi”, ameongeza Mhandisi 
Lydia.
Amesema,
 halmashauri hiyo inapaswa kuhakikisha inatekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa
 wa Singida Dkt Rehema Nchimbi la kuongeza asilimia ya upatikanaji wa 
maji katika halmashauri hiyo kutoka 45 hadi 72 ifikapo mwezi Juni, 2018 
pamoja na kuandaa takwimu sahihi za upatikanaji wa maji ifikapo Disemba 
mwaka huu.
Mhandisi
 Lydia amefafanua kuwa halmashauri hiyo itaweza kuongeza asilimia ya 
upatikanaji maji na kufikia lengo la asilimia 72 endapo watendaji wote 
hasa wajumbe wa timu ya usimamizi wa sekkta ya maji, watashirikiana 
kusimamia ujenzi wa miradi mitano pamoja na ukarabati wa miradi minne 
iliyopo kwenye bajeti.
“Kila
 Mjumbe hapa ana kazi ya kufanya katika miradi hii ya Makanda, Nyaranga,
 Kikombo, Makutopola na Kicheho inayojengwa pamoja na ile ya Sanza, 
Mkwese, Londoni na Sorya inayokarabatiwa, Kitengo cha ugavi kisimamie 
taratibu za manunuzi zinafuatwa pamoja na kuhakiki ubora wa mkandarasi, 
mwanasheria aelekeze taratibu za kisheria, Maendeleo ya jamii ahakikishe
 wananchi wanaujua mradi vizuri, kila mmoja akitekeleza jukumu lake 
ipasavyo tutafikia lengo”, ameeleza na kuongeza kuwa,
“Idara
 ya maji msifanye siri miradi ya maji na kujifungia wenyewe hakikisheni 
timu hii ya usimamizi wa sekta yenu inafahamu vizuri miradi yote ya maji
 pamoja na kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo, mkifanya hivyo mtaenda 
kwa kasi na kazi itafanyika kwa ufanisi, sio kila kitu mfanye wenyewe 
tu”, ameongeza Mhandisi Lydia.
Aidha
 Mhandisi Lydia amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya 
Manyoni Charles Fussi kwa kujitoa kwake katika kusimamia na kutoa fedha 
za kusaidia miradi ya maji akitoa mfano wa kiasi cha milioni 16 
zilizotolewa na mkurugenzi huyo kutoka katika makusanyo ya ndani kwa 
ajili ya ujenzi wa mradi wa maji.
Naye
 Mhandisi wa Maji kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Athanas Nziku ameieleza 
timu hiyo kuwa usimamizi wa jumuiya za watumia maji ni jambo muhimu 
kwakuwa takwimu zimeonyesha jumuiya hizo zimekuwa zikikusanya pesa 
nyingi sambamba na matumizi makubwa ya fedha wanazokusanya.
Mhandisi
 Nziku amewafafanulia kuwa jumuiya hizo za watumia maji zinapokusanya 
fedha nyingi sambamba na kutumia fedha nyingi ni moja ya kiashiria kuwa 
miradi hiyo ya maji inaweza kufa hivyo wazitembelee na kuona tatizo liko
 wapi endapo liko ndani ya uwezo wa halmashauri liweze kutatuliwa 
mapema.
Kwa
 upande wake Diwani wa Kata ya Mkwese na Mwenyekiti wa huduma za Jamii 
wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Robert Kenze amesema, halmashauri 
hiyo imedhamiria kuboresha huduma za maji ambapo ajenda ya maji imewekwa
 kipaumbele katika vikao vyote muhimu.

0 comments:
Post a Comment