Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amezitaka halmashauri za Mkoa wa 
Singida kuacha kulalamika kukosa mapato bali watumie vizuri rasilimali 
nyingi zilizopo, ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuongeza mapato yao. 
Dkt
 Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akifungua mafunzo ya 
kutambua fursa na vikwazo kwa ajili ya kupanga miradi ya maendelo kwa 
jamii (O&OD) yaliyoandaliwa na ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na 
Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa watendaji wa halmashauri zote za 
mkoa wa Singida. 
Amesema
 Mkoa una fursa nyingi katika sekta ya kilimo, utalii, ufugaji, madini 
na uvuvi ambazo bado hazijatumiwa vizuri na halmashauri katika kukuza 
uchumi wa viwanda kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa wa Singida. 
“Singida
 ina zalisha Vitunguu vingi na bora nchini, ina zalisha viazi zitani 
vingi na vyenye ubora, singida pia ni mzalishaji mkubwa wa alizeti na 
mafuta ya alizeti huku tukiwa na viwanda zaidi a 120 vya kusindika 
mafuta ya alizeti, katika sekta ya utalii tuna vivuti vngi ikiwemo bwawa
 la kuongelea ‘swimming pool’ lililojengwa na mjerumani na lipo katikati
 ya pori lakini vyote hivi hatujavitumia vizuri,” amesisitiza Dkt 
Nchimbi.
Dkt
 Nchimbi ameongeza kuwa halmashauri zinapaswa kutotumia mafunzo hayo 
kulalamika bali mafunzo hayo yawajengee uwezo wa kutambua wapi kuna 
pengo katika maendeleo ya jamii na kisha kuanisha fursa na mikakati ya 
kuzitumia fursa hizo kuziba pengo hilo. 
Aidha
 amewataka kutumia fursa ya malengo na mitazamo waliyonayo ambayo 
inaweza kuleta maendeleo pamoja na kuhakikisha kuwa mafunzo hayo 
yanawajengea uwezo wa kubaini na kuitumia ajenda ya fursa na vikwazo 
katika maendeleo kwa ngazi zote. 
Dkt
 Nchimbi amesema matarajio yake ni kuona kila mshiriki wa mafunzo hayo 
ana mabadiliko ya tabia katika utendaji wake ambapo mabadiliko hayo 
yanaweza kupimika aidha kwa macho au viashiria vingine.
Ameongeza
 kuwa matarajio ya mengine ni kuwa na Singida mpya yenye takwimu sahihi 
za bidhaa zote zinazozalishwa Mkoani Singida ili kuzitumia takwimu hizo 
katika kupanga mikakati ya maendeleo pamoja na kutangaza fursa zote 
zilizopo Mkoani hapa. 
Dkt
 Nchimbi ameeleza kuwa mafunzo hayo wamepatiwa ili kutatua changamoto 
zilizopo na endapo kutaendelea kuwepo kwa changamoto hizo katika sekta 
mbalimbali ikiwemo za kilimo, afya, maji, elimu, barabara na utawala 
bora basi tumi nzima ya fursa na vikwazo itakuwa imeshindwa. 

0 comments:
Post a Comment