Home » » TUNAZO RASILIMALI NYINGI LAKINI BADO KUNA HALMASHAURI ZINALALAMIKA HAKUNA MAPATO; DKT NCHIMBI.

TUNAZO RASILIMALI NYINGI LAKINI BADO KUNA HALMASHAURI ZINALALAMIKA HAKUNA MAPATO; DKT NCHIMBI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amezitaka halmashauri za Mkoa wa Singida kuacha kulalamika kukosa mapato bali watumie vizuri rasilimali nyingi zilizopo, ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuongeza mapato yao.
Dkt Nchimbi ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akifungua mafunzo ya kutambua fursa na vikwazo kwa ajili ya kupanga miradi ya maendelo kwa jamii (O&OD) yaliyoandaliwa na ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa watendaji wa halmashauri zote za mkoa wa Singida.
Amesema Mkoa una fursa nyingi katika sekta ya kilimo, utalii, ufugaji, madini na uvuvi ambazo bado hazijatumiwa vizuri na halmashauri katika kukuza uchumi wa viwanda kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa wa Singida.
“Singida ina zalisha Vitunguu vingi na bora nchini, ina zalisha viazi zitani vingi na vyenye ubora, singida pia ni mzalishaji mkubwa wa alizeti na mafuta ya alizeti huku tukiwa na viwanda zaidi a 120 vya kusindika mafuta ya alizeti, katika sekta ya utalii tuna vivuti vngi ikiwemo bwawa la kuongelea ‘swimming pool’ lililojengwa na mjerumani na lipo katikati ya pori lakini vyote hivi hatujavitumia vizuri,” amesisitiza Dkt Nchimbi.
Dkt Nchimbi ameongeza kuwa halmashauri zinapaswa kutotumia mafunzo hayo kulalamika bali mafunzo hayo yawajengee uwezo wa kutambua wapi kuna pengo katika maendeleo ya jamii na kisha kuanisha fursa na mikakati ya kuzitumia fursa hizo kuziba pengo hilo.
Aidha amewataka kutumia fursa ya malengo na mitazamo waliyonayo ambayo inaweza kuleta maendeleo pamoja na kuhakikisha kuwa mafunzo hayo yanawajengea uwezo wa kubaini na kuitumia ajenda ya fursa na vikwazo katika maendeleo kwa ngazi zote.
Dkt Nchimbi amesema matarajio yake ni kuona kila mshiriki wa mafunzo hayo ana mabadiliko ya tabia katika utendaji wake ambapo mabadiliko hayo yanaweza kupimika aidha kwa macho au viashiria vingine.
Ameongeza kuwa matarajio ya mengine ni kuwa na Singida mpya yenye takwimu sahihi za bidhaa zote zinazozalishwa Mkoani Singida ili kuzitumia takwimu hizo katika kupanga mikakati ya maendeleo pamoja na kutangaza fursa zote zilizopo Mkoani hapa.
Dkt Nchimbi ameeleza kuwa mafunzo hayo wamepatiwa ili kutatua changamoto zilizopo na endapo kutaendelea kuwepo kwa changamoto hizo katika sekta mbalimbali ikiwemo za kilimo, afya, maji, elimu, barabara na utawala bora basi tumi nzima ya fursa na vikwazo itakuwa imeshindwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa