Home » » Singida Walivyoadhimisha Siku Ya Habari

Singida Walivyoadhimisha Siku Ya Habari


DAS wilaya Iramba Singida, Yahaya Anania, akikabidhi sehemu ya msaada wa thamani ya zaidi ya Milioni moja


Wahadzabe wakisubiri msaada kutoka kwa klabu ya wanahabari mkoa Singida(SINGPRES0, walipotembelea ili kutoa msaada
Seif Takaza (kushoto), Mwenyekiti wa klabu ya wanahabari mkoa Singida akikabidhi sehemu ya msaada wa kibinadamu kwa katibu tawa

Singida,
Mei 04, 2012.
WANAHABARI mkoa Singida, kupitia klabu yao SINGPRESS,  wameungana na wanahabari wenzao duniani kwa kuadhimisha siku yao kwa kutoa msaada wa kibinadamu kwa jamii ya Wahadzabe wanaoishi kitongoji cha Kipamba, kata Mwangeza, wilayani Iramba.
Katika kuadhimisha siku hiyo, SINGPRESS imetoa msaada wa chakula na vifaa vya shule vyenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni moja.
Msaada huo ulikabidhiwa kwa mgeni rasmi, katibu tawala wa Wilaya Iramba, Yahaya Anania, kabla naye kumkabidi mwenyekiti wa kitongoji hicho, Edward Mashimba, ili kwa kushirikiana na wajumbe wa serikali ya kijiji, viwafikie walengwa waliokuwepo katika hafla hiyo.
Akipokea msaada huo, Anania aliwashukuru wanahabari, kutokana na kuithamini jamii hiyo, inayoishi maisha ya shida, kwa kuhamahama porini, huku chakula chao kikuu kikiwa ni mizizi, matunda na nyama pori, ambavyo hata hivyo hivi sasa imekuwa shida, kutokana na kuingiliwa na jamii ya wafugaji katika eneo lao.
Hata hivyo, katibu tawala huyo amesema serikali kwa kushirikianana wadau mbalimbali, imekuwa ikitoa misaada ili kuinusuru jamii na maisha ya shida.
Alisema tayari serikali imetenga eneo lo na kulifanya kuwa hifadhi maalumu, lakini pamoja na jitihada hizo, bado jamii ya wafugaji imeingilia makazi yao na kuanza kufyeka msitu ovyo katika makazi yao.
Kutokana na hali hiyo, katibu tawala huyo ameitaka jamii hiyo kuwafichua wote wanaoharibu mazingira, katika kipindi hiki ambacho taratibu zinaendelea kuwatoa wote waliovamia eneo lao.
Mapema mwenyekiti wa SINGPRESS, Seif Takaza, alimweleza mgeni rasmi kuwa, wanahabari wa Singida badala ya kuadhimisha siku yao mjini, walionelea vyema kwenda katika jamii hiyo ili watoe sauti yao ambayo itasikika katika jumuiya mbalimbali ndani na nje, waweze kusaidiwa.
“Sisi tumeona badala ya kuadhimisha siku hii mjini Singida, tumeona tuje kwenu tuwaletee hiki kidogo na jamii ingine ielewe matatizo yenu…..kuliko hivi mnavoishi miaka yote, lakini hakuna mabadiliko yoyote, naamini tutaungwa mkono na wengi,”alisema.
Msaada huo uliungwa mkono kwa kupigwa jeki na mfanyabiashara maarufu wa mjini Singida, Bw. Nagji, ambaye alijitolea katoni kadhaa za sabuni ya kufulia, Biskuti, madaftari na pipi, ili kuisaidia jamii hiyo.
Na Elisante John 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa