Home » » DKT. KONE ATOA ONYO LA KUTOKUPOKEA WALIMU WASIO NA WITO MKOANI SINGIDA.

DKT. KONE ATOA ONYO LA KUTOKUPOKEA WALIMU WASIO NA WITO MKOANI SINGIDA.




Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone akizungumza kwenye kilele cha mahafali ya tano ya chuo cha walimu mjini Singida. Kulia ni Mkuu wa chuo hicho cha walimu Didas Monyo.
Mkuu wa chuo cha walimu cha Singida mjini Didas Monyo akitoa taarifa yake kwenye mahafali ya tano ya chuo hicho. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone.
Baadhi ya wanachuo wa chuo cha ualimu cha Singida mjini waliohudhuria mahafali ya tano.
Bango la chuo cha ualimu na shule ya sekondari ya Singida iliyopo mjini Singida. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na.Nathaniel Limu.
Serikali ya mkoa wa Singida imedai kwamba haina nafasi kabisa ya kupokea walimu ambao hawana maadili ya ualimu kwa hofu kwamba wanamadhara makubwa katika ustawi wa sekta ya elimu.
Akizungumza kwenye mahafali ya tano ya chuo cha ualimu cha Singida mjini, Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone  amesema  kupokea walimu ambao hawana maadili ya ualimu, kuna hasara nyingi tena kubwa, zikiwemo kushusha taaluma na kuchangia kuharibu maadii ya wanafunzi.
 Kuhusu wahitimu walimu tarajiwa hao 559, Dkt. Kone amesema anafahamu kuwa watakuwa wamechagua au kuchaguliwa kwenda kufanya kazi ya ualimu katika mikoa mbali mbali ya Tanzania , ikiwemo mkoa wa SIngida.
Awali mkuu wa chuo cha ualimu Singida Didas Monyo, alitaja changamoto mbali mbali zinazokikabili chuo hicho, kuwa ni pamoja na upungufu wa vitabu vya kufundishia (kiada) na uhaba mkubwa wa maji.
 Kwa mujibu wa mwalimu Monyo chuo hicho kina wanahcuo 1,610, kati yao wapo wa mwaka wa kwanza 1051 na wa mwaka wa pili ambao ndio wahitimu ni 559.
Kwa hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa