Home » » AJALI ILIYOHUSISHA MAGARI MATATU KWA MPIGO MKOANI SINGIDA.

AJALI ILIYOHUSISHA MAGARI MATATU KWA MPIGO MKOANI SINGIDA.

Askari wa usalama barabarani mjini Singida, wakipima ramani sehemu ya ajali iliyohusisha Tipper T.733 BGX ambalo lilikuwa likiendeshwa na Adam Awadhi (amevunjika miguu yote) likitokea maeneo ya Mwenge kuja mjini kati kupitia barabara ya Singida – Arusha, liligonga kwa nyuma fuso.T.780 AFR. Fuso hilo  lilikuwa likielekea barabara ya Stanley Motel ambapo baada ya kugongwa liliangukia gari ndogo T.491 ARG.Dereva wa fuso lililokuwa limebeba sukari guru na dereva wa gari hilo amelazwa hospitali ya mkoa ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Tipper T733 BGX  likiwa limegongana na fuso namba T780 AFR.
Baadhi ya wakazi wa Singida mjini wakishuhudia ajali iliyohusisha magari matatu jana  saa 9.20 alasiri.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Kwa hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa