Home » » MH. TUNDU LISSU AFANANISHA KESI YAKE NA MKASA WA YOHANA MBATIZAJI.

MH. TUNDU LISSU AFANANISHA KESI YAKE NA MKASA WA YOHANA MBATIZAJI.


Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki kupitia Chama cha CHADEMA Mh. Tundu Lissu (mwenye fimbo) akiingia kwenye viwanja vya kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida kwa kuhutubia wananchi.
Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CHADEMA) muda mfupi kabla hajaanza kuhutubia wakazi wa jimbo la Singida mjini. Wa kwanza kulia ni mke wake.
Mbunge wa viti maalum kupitia Chama cha CHADEMA na ambaye ni mdogo wake Tundu Lissu Christina Mughwai, akisalimia mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya Tundu.
Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CHADEMA) Mh. Tundu Lissu akihutubia wakazi wa jimbo la Singida mjini.
Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CHADEMA) Mh. Tundu Lissu (waliosimama mwenye kofia) akitoa salamu ya CHADEMA ya ‘peoples power’. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (CHADEMA) Mh. Tundu Lissu, amedai kwamba zaidi ya shilingi milioni 200, zimetumika kugharamia kesi ya ‘kuunga unga’ ambayo ililenga kutafuta kichwa chake kama ilivyokuwa kwa Yohana Mbatizaji.
Bila kufafanua kuwa kichwa chake kilikuwa kikitafutwa kikiwa kimetenganishwa na kiwiliwili au kikiwa hakijatenganishwa na kiwili wili chake, amesema kati ya kesi 14 zilizofunguliwa katika mahakama tofauti nchini, kwa ajili ya kutengua matokeo ya wabunge wa CHADEMA ya kwake ilikuwa kubwa zaidi na ndio maana haikupewa umuhimu unaostahili  na vyombo vya habari.
Hata hivyo, hakufafanua au kueleza iwapo hivyo vyombo vya habari navyo vilinufaika na kiasi hicho cha shilingi milioni 200 ambazo zililenga kumwangamiza kisiasa.
Tundu amesema wana-CCM hao ambao ni wakulima wa kawaida, wametumiwa na wahusika walikuwa wakimwaga fedha ili kufanikisha azma zao ya kumng’oa katika nafasi yake  ya ubunge, lakini fedha zote zimeliwa bila kufanikisha lengo.
Aidha, alisema kuwa aliyekuwa katibu mkuu wa CCM Yusufu Makamba, aliwahi kutoa waraka kuwa katika majimbo yote yaliyochukuliwa na vyama vya upinzani,wahusika walioshindwa,wafungue kesi mahakamani.
Habari kwa Hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa