Home » » WAJASIRIAMALI SINGIDA WANUFAIKA NA MRADI WA KUWEZESHA BIASHARA.

WAJASIRIAMALI SINGIDA WANUFAIKA NA MRADI WA KUWEZESHA BIASHARA.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Parseko Kone (kushoto) akitembelea maonyesho ya wajasiriamali mara baada ya kufungua sherehe za utoaji zawadi kwa washindi wa mashindano ya mpango huo zilizofanyika katika ukumbi wa chuo cha FDC mjini Singida.
Na.Mwandishi wetu
Akiongea Mkuu wa mkoa amesema kuwa washiriki hao walinufaika na mtaji wa Sh. 2,800,000, BDG ilitumia kigezo cha ustawi wa biashara na uandishi mzuri wa michanganuo katika kuwapatia wajasiriamali hao fedha hizo.
Aidha amesema tangu mpango huo uanzishwe mwezi Agosti 2008, umewapatia wajasiriamali nchini, mtaji wenye thamani ya Sh. Bilioni 15 hadi kufikia Agosti mwaka jana.
Kone amepongeza wajasiriamali hao ambao jumla yao ni watu 64, kwa kushinda na kufanikiwa kupeleka fedha hizo mkoani Singida, ambazo amesema anaamini zitasaidia kuongeza mzunguko wa fedha.
 Habari kwa Hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa