Home » » Mtumishi wa Usalama Taifa ajinyonga

Mtumishi wa Usalama Taifa ajinyonga



Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,
Celina Kaluba
Mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa mkoa wa Singida amejinyonga hadi kufa, akiwa kwenye eneo lake la kazi, kwa kutumia shuka.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Celina Kaluba, alimtaja mtumishi huyo kuwa ni Azaria Mbaga (47), mkazi wa Sabasaba mjini Singida.

Kamanda Kaluba alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 9, mwaka huu saa 8:30 usiku katika kibanda kinachotumiwa na walinzi wa ofisi hiyo, iliyopo eneo la Bomani, mjini Singida.

Alisema kuwa, muda mfupi baada ya kujinyonga, wenzake walifanikiwa kuuona mwili wake ukiwa umening’inia ndani ya banda hilo, majira ya saa 9:30 usiku, na kutoa taarifa kituo cha Polisi.




Kaluba alisema marehemu katika miaka ya nyuma, aliwahi kuugua maradhi ya akili na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), ambako alipatiwa tiba na kupona.


”Marehemu siku kama tatu au nne hivi, kabla ya kujinyonga, alionekana kama vile amechanganyikiwa, nadhani hali hiyo ilikuwa dalili za kumsababishia ajiue kwa kujinyonga,” alisema Kaluba.


Alisema chanzo kamili cha kujinyonga kwake, hakijafahamika, lakini upelelezi zaidi kuhusiana na tukio hilo unaendelea.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa