Home » » BALOZI SEIF IDD APIGA TAFU SKULI YA SEKONDARI YA MASISTA YA MITUNDURUNI MKOANI SINGIDA.

BALOZI SEIF IDD APIGA TAFU SKULI YA SEKONDARI YA MASISTA YA MITUNDURUNI MKOANI SINGIDA.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi mchango wa shilingi 1,000,000/- Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki Mh. Dianna Chilolo kwa ajili ya uendelezaji wa Jengo Jipya la Skuli ya Sekondari ya Masista ya Mitundu Mkoani Singida. Mchango huo aliukabidhi VIP Karimjee Mjini Dar es salaam kutekeleza ahadi aliyoitowa wakati alipotembelea Ujenzi huo Tarehe 7/2/2012 Huko Singida akiwa mlezi wa Mkoa huo Kichama.
Othman Khamis Ame – Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amekabidhi mchango wa Shilingi Milioni Moja { 1,000,000/-} kwa ajili ya uendelezaji wa Ujenzi wa Jengo jipya la Skuli ya Sekondari ya Masista iliyopo Mitundu Mkoani Singida.
Mchango huo ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa alipotembelea Ujenzi wa Jengo hilo wakati wa ziara yake ya siku tatu Mkoani Singida ya tarehe 7 February mwaka 2012 akiwa Mlezi wa Mkoa huo Kichama.
Balozi Seif amekabidhi Mchango huo kwa Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki Mh. Dianna Chilolo hapo katika Ofisi ya watu Mashuhuri { VIP } iliyopo katika jengo la  Karimjee Mjini Dar es salaam.
Akitoa mchango huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema  amelazimika kutoa mchango huo kutokana na uamuzi wa Uongozi wa Skuli hiyo kutoa upendeleo wa kuwapatia Elimu  bila ya ada Watoto Yatima na wale wanaoishi  katika Familia zenye mazingira magumu.
Akipokea Mchango huo Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki Mh. Dianna Chilolo amempongeza Balozi Seif kwa Jitihada zake za kuunga mkono Maendeleo ya Elimu Mkoani Singida.
Alisema Mchango huo ni moja ya Vitendo vinavyoendelea kuwapa moyo Wananchi wa Singida katika  harakati zao za kupewa msukumo wa Kimaendeleo wakati wanapoanzisha Miradi ya Utawi wa Jamii.
Mh. Dianna Chilolo ameahidi kwamba mchango alioutoa Balozi Seif ataufikisha kwa wakati muwafaka na kutumiwa kwa lengo lililokusudia.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif aliutembelea Mkoa wa Singida mnamo Mwezi wa Pili mwaka huu katika ziara ya siku tatu akiwa mlezi wa Mkoa huo Kichama.
Balozi Seif katika ziara hiyo alibahatika kuweka Mawe ya Msingi pamoja na kuzindua miradi tofauti ya Maendeleo na Kiuchumi ya Wananchi wa Singida ikiwemo pia ile ya Chama Cha Mapinduzi.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa