Home » » TUNDU LISSU ASHINDA KESI YA KUPINGA UBUNGE WAKE

TUNDU LISSU ASHINDA KESI YA KUPINGA UBUNGE WAKE

 

  • Hoja zote za upande wa mlalamikaji zatupwa.
  • Maofisa Jeshi pamoja na kikosi maalum waudhulia maakamani.

Mbunge
wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu, ameshinda kesi
iliyofunguliwa dhidi yake mjini Singida kupinga ushindi uliomweka
madarakani

Hukumu
imetolewa na Jaji Moses Mzuna anayetoka mahakama kuu kanda ya
Kilimanjaro, iliyofunguliwa na makada wawili wa CCM, Shabani Itambu na
Pascal Hallu.
 
Leo
mahakamani wafuasi wa vyama mbalimbali vya siasa, wananchi wa Singida,
na waandishi wa habari walijitokeza kwa wingi sana katika eneo la
mahakama.


Idadi
ya Polisi pia ilikuwa kubwa, ndani na nje ya mahakama.Kilicho kuwa cha
ajabu kidogo leo getini maofisa wote wakubwa wa jeshi la polisi
walikuwepo pale na kikosi maalumu kwa ajili ya kukagua kila anayeingia
mahakamani,  kila mtu aliyekuwa anaingia mahakamani alipekuliwa hadi
wabunge waliokuja kusikiliza kesi hiyo.


Akisoma
hukumu Jaji Moses Mzuna alisema “HOJA YA TISA, Kama Mgombea wa
walalamikaji (CCM) alikataa kusaini matokeo. Hoja hii haipaswi
kunipotezea muda sana. Njau hakuhudhuria, aliwakilishwa na mlalamikaji
wa kwanza ambaye alikataa kusaini matokeo.


Wakili
wa serikali alisema, kukataa pekee kusaini matokeo hakusaidii kutengua
matokeo. Hivyo hata hoja ya tisa naitupilia mbali. Haikuwa sahihi.

Hoja
ilitolewa hapa, kuwa mawakala walikula kiapo kwa hakimu. Walalamikaji
walisema kuwa walipaswa kula kiapo kwa msimamizi wa uchaguzi. Je
kuapishwa na hakimu kunabatilisha matokeo?


Hoja
zilizotolewa na mawakili wa serikali walisema Hakimu ana mamlaka ya
kutoa viapo. Binafsi nasema kuwa waliotunga sheria hawakumaanisha kuwa
Mahakimu hawaruhusiwi kuapisha mawakala, vinginevyo kungekuwepo fomu ya
hakimu tu. Lakini fomu zinaonyesha hakimu, Msimamizi wa uchaguzi na
Msimamizi msaidizi, fomu inatambulika kisheria, kwa sheria ya Uchaguzi.
Hii haihusiani na zoezi la uchaguzi.


Katika kesi ya Prince bagenda Vs Wilson masilingi, katika kesi hii mawakala walifanya kazi bila kuapishwa, na ilichukuliwa kuwa sehemu ya kutengua uchaguzi, angalia pg 240.


Kwa
lugha yake jaji alisema hawakuwa na mamlaka halali, lawful mandate,
lakini ilisaidia kutengua, na mwanasheria wa serikali alihusika katika
hili.


Maelezo
hayo yanatofautiana na kesi iliyo mbele yangu, jimbo la Singida
mashariki mawakala walikula kiapo, na walikuwa na mamlaka halali. Hivyo
hoja hii naitupilia mbali


HIVYO, UCHAGUZI ULIKUWA WA HAKI, NA TUNDU LISSU NI MBUNGE HALALI NA UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA WA WA HAKI, HIVYO SIWEZI KUTENGUA.


Walalamikaji
wa kesi hiyo, iliyofunguliwa mahakama kuu kanda ya Dodoma, walikuwa
wanatetewa na wakili Godfrey Wasonga, kutoka mkoani Dodoma, huku Lissu
akijisimamia mwenyewe.


Kesi
hiyo ilianza kusikilizwa Machi 12, 2012, kufuatia makada wawili wa CCM,
kupinga ushindi wa Lissu kwa madai kuwa uchaguzi huo uligubikwa
na dosari nyingi.


Awali
Katika mahojiano na Lissu, alisema vyovyote mahakama itakavyo
hukumu, anajivunia kuimarisha demokrasia na kuwa mbunge wa kwanza
kutoka upinzani, kwenye historia ya mikoa ya kanda ya kati.Habari kwa Hisani ya Media 2 Solution Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa