Home » » BODI ZA ZABUNI SINGIDA ZATAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA YA MWAKA 2004.

BODI ZA ZABUNI SINGIDA ZATAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA YA MWAKA 2004.


Mwanasheria Mwandamizi wa PPAA Esthery Nyagawa akitoa mada yake kwenye warsha iliyohudhuriwa na wazabuni, wahasibu na maafisa ugavi (hawapo kwenye picha) iliyohusu  utatuzi wa migogoro katika ununuzi wa umma chini ya sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2004 na sheria mpya ya mwaka 2011.
 Baadhi ya wazabuni, maafisa ugavi kutoka serikalini na wahasibu waliohudhuria warsha iliyohusu utatuzi wa migogoro katika manunuzi ya umma. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mwanasheria Mwandamizi wa mamlaka ya rufaa za zabuni za umma (PPAA) Esthery Nyagawa, amezihimiza bodi za zabuni kuwa makini wakati wa uteuzi wa zabuni ili kujijengea mazingira mazuri ya kuteua mzabuni ambaye atatoa huduma bora inayofanana na thamani ya fedha atakazolipwa.
Nyagawa ametoa changamoto hiyo wakati akitoa mada yake ya matatizo yaliyiokithiri katika  ununuzi wa umma, ambayo husababisha malalamiko kutoka kwa zabuni.
Amesema baadhi ya bodi za zabuni, zimekuwa zikiteua wazabuni wasiokuwa na sifa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa makini  na hivyo  kuisababishia serikali au taasisi ya umma, kupoteza fedha nyingi.
Mwanasheria huyo amesema jambo la msingi ni bodi za zabuni kuzingatia sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2004, inayoelekeza jinsi mchakato wa ununuzi wa umma unavyopaswa kuendeshwa.
Katika hatua nyingine, Nyagawa amewataka wazabuni wasikubali kuanza utekelezaji wa mkataba, bila ya kuwa na mkataba.
Aidha, amesema wazabuni wanalo jukumu kubwa lakutoa taarifa juu ya matatizo wanayokumbana nayo wanaposhiriki kwenye zabuni za serikali na taaisisi zake, ili yaweze kufanyika na kushughulikiwa ipasavyo.
Mwanasheria huyo mwandamizi, ametoa mada hiyo kwenye warsha kuhusu utatuzi wa migogoro katika ununuzi wa umma chini ya sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2004 na sheria mpya ya mwaka 2011.
Warsha hiyo ilihudhuriwa na wazabuni wa huduma mbalimbali, wakuu wa taasisi za umma, maafisa ugavi wa serikali na wahasibu. 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa