
 Katibu  tawala mkoa wa Singida (kulia) akikabidhi mbuzi watatu wakiwa ni zawadi  kutoka kwa Rais Kikwete kwa wazee wasiojiweza wa kambi ya Sukamahela  wilayani Manyoni.

 Katibu  tawala mkoa wa Singida Liana Hassan (kulia) akikabidhi dumu la mafuta  ya alizeti moja ya zawadi zilizotolewa na Rais Kikwete kwa wakazi wa  kambi ya wazee ya Sukamahela.

 Katibu tawala mkoa wa Singida Liana Hassan (kulia) akimvisha shati mmoja wa wakazi wa kambi ya wazee ya Sukamahela.
 Katibu  tawala mkoa wa Singida,Liana Hassan akizungumza kwenye hafla ya  kukabidhi zawadi zilizotolewa na Rais Jakaya Kikwete, kwa wakazi wa  kambi ya Sukamahela wilayani Manyoni.Kushoto ni mkurugenzi wa  halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Fotunata Malya na anayefuata ni mke wa  Ras, Liana Hassani.

Mkazi  wa kambi ya wazee wasiojiweza ya Sukamahela wilayani Manyoni Kareudia  Madoli akitoa shukurani kwa niaba ya wenzake kwa Rais Kikwete kwa msaada  wake kwa ajili ya sherehe ya pasaka.Picha zote na Nathaniel Limu
---
Katibu  tawala mkoa wa Singida,Liana Hassan amewahimiza  wakazi mkoani humo  kujenga utamaduni wa kusaidia makundi ya watu wenye mahitaji ili pamoja  na mambo mengine kuwapunguzia makali ya maisha.
Liana  ametoa wito huo wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi zawadi  mbalimbali zilizotolewa na Rais Jakaya Kikwete, kwa wakazi wa kambi ya  Sukamahela wilayani Manyoni.Msaada huo ni kwa ajili ya wakazi hao, kusheherekea pasaka.
Alisema upo  umuhimu mkubwa kwa wakazi mkoani humo, kutambua kwamba wana wajibu wa  kusaidia kwa hali na mali,makundi mbalimbali yenye mahitaji wakiwemo  wazee wasiojiweza.
“Kwa hiyo  ndugu zangu nawaombeni sana tumuunge mkono rais wetu Kikwete katika  kuyasaidia makundi haya.Mwaka jana rais Kikwete alitoa msaada kwa watoto  waishio kwenye mazingira magumu cha kituo cha Kititimo, na leo hii  anawasaidia wakazi wa kambi hii ya Sukamahela”,alisema na kuongeza;“Hebu kila  mmoja wetu kwa kadri ya uwezo wake utakavyomuruhusu,tumuunge rais kwa  kuyasaidia makundi haya wakati wa sherehe mbalimbali na hata siku za  kawaida”.
Awali afisa  jamii mfawidhi wa makazi ya Sukamahela,Fredrick Mbyoya alitaja baadhi  ya changamoto zinazoikabili kambi hiyo, kuwa ni uhaba wa maji,wakazi  hawajapata mavazi kwa muda mrefu na watoto wanaosoma Day care  centre,shule ya msingi na sekondari,hawana viatu,sare,madaftari na  kalamu.Kwa mujibu wa Mbyoya, kituo hicho kina wakazi 73 na nyumba za kuishi 54.
Zawadi  zilizotolewa na rais kwa wakazi wa kambi ya Sukamahela, ni mchele kilo  112,lita 40 za mafuta ya alizeti na beberu (mbuzi) tatu wakubwa.Pia  ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida,imemuunga mkono rais kwa kutoa msaada  wa nguo mbalimbali kwa wakazi hao ambao baadhi,ni wagonjwa wa ukoma.Wakati huo  huo, tarehe (7/4/2012) mbunge wa jimbo la Manyoni mashariki,John  Chiligati,alitarajiwa kuwasaidia wakazi wa Sukamahela mchele kilo  100,mbuzi wawili na mafuta ya alizeti lita 20.
  
Lengo la msaada ni kuwawezesha wakazi hao kufurahia sikukuu ya pasaka.Pia Chiligati,alitarajiwa kuwasaidia wazee wasiojiweza wa Majengo Manyoni mjini,mchele kilo 20,mbuzi moja na mafuta ya alizeti,lita kumi.
Lengo la msaada ni kuwawezesha wakazi hao kufurahia sikukuu ya pasaka.Pia Chiligati,alitarajiwa kuwasaidia wazee wasiojiweza wa Majengo Manyoni mjini,mchele kilo 20,mbuzi moja na mafuta ya alizeti,lita kumi.

0 comments:
Post a Comment