Katibu wa CCM Mkoa wa Singida 
Naomi Kapambala aaizungumza na waanndishi wa habari juu ya ufafanuzi wa 
maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo.
Na Hillary Shoo, Singida
Mbunge wa Jimbo la Singida mjini 
(CCM), Mohammed Dewji ameulalamikia uongozi wa Chama chake Mkoa wa 
Singida kwa kitendo cha kuchelewesha mchakato wa kumalizia ujenzi wa 
Uwanja wa michezo Namfua  ikiwa ni moja ya ahadi zake alizotoa kwa 
wananchi wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
Kuchelewa huko kuanza kwa mchakato 
wa ukarabati na uwekaji wa nyasi za bandia kwenye uwanja huo imeelezwa 
ni kutokana na urasimu na maslahi binafsi  miongozi mwa viongozi wa CCM 
Mkoa wa Singida.
Katika barua yake ya Julai 31 mwaka 
huu kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Dewji amedai kuwa kwa 
kiasi kikubwa ameweza kutekeleza Ilani ya Uchaguzi kwa vipindi vyote 
viwili pamoja na ahadi zake binafsi, isipokuwa ahadi ya kumalizia ujenzi
 wa michezo Namfua.
Katika barua hiyo, ambayo pia 
ameinakili kwa Rais Jakaya Kikwete, Katibu Baraza la wadhamini CCM 
Taifa, Katibu wa Uchumi na Fedha na Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Dewji
 amedai kuwa kila alipotaka kufanya hivyo alipata vikwazo kutoka kwa 
viongozi wa CCM mkoa wa Singida.
Katikati ya kiwanja chenyewe.
Amesema kuwa matayarisho yote muhimu
 kuhusiana na ujenzi huo yapo tayari, ikiwa ni pamoja na kuwepo dola za 
kimarekani 880,000 (sawa na sh bilioni 1.46) ambazo kwa kushirikiana na 
Rais Kikwete aliweza kuzipata kutoka Makampuni ya Airtel Tanzania na 
Mohammed Ent (T) Ltd.
Dewji amesema wakati wa kampeni za 
uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 yeye pamoja na Raisi Jakaya Kikwete walitoa 
ahadi ya kukarabati na kuweka nyasi za bandia 
kwenye uwanja huo unaomilikiwa na chama cha mapinduzi CCM.
Hili ni jukwaa kuu la uwanja wa Namfua unaomilikiwa na CCM Mkoa wa Singida.
 “Baada ya uchaguzi  sote wawili 
tulishinda na sasa tunatumikia wananchi, na kwa kiasi kikubwa 
tumefanikiwa kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa vipindi vyote viwili, 
pamoja na ahadi zetu binafsi, lakini ahadi tuliyotoa ya ukarabati wa 
uwanja mpaka sasa hatujafanikiwa kuitekeleza. Alisem MO na kuongeza
Dewji amesema anasikitishwa   na 
uongozi wa CCM Mkoa wa Singida bila sababu za msingi wanachelewesha 
kuanza kwa mchakato wa ukarabati wa uwanja huo.
Aidha amesema kuna vikao vingi 
viimefanyika na makampuni hayo bila mafanikio na hivyo anaomba CCM Makao
 makuu kuingilia kati ili kama kuna jambo linasababisha kusuasua kwa 
mchakato huo liweze kupatiwa ifumbuzi na ukarabati ufanyike haraka 
iwezekanavyo.
Vijana wakicheza mpira uwanjani humo.
Amesema suala la uchakavu wa uwanja 
wa Namfua imekuwa ni kero kubwa inayowakabili wananchi wa jimbo la 
singida mjini kwa sasa na hivyo kuwanyima vijana fursa za kutumia uwanja
 huo ili kupata ajira na kukuza vipaji kwa vijana.
Kutokana na ukweli kwamba muda wa 
kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 unayoyoma, Dewji maarufu kwa jina la "MO" 
amemwomba Katibu Mkuu wa CCM kuingilia kati urasimu huo usio wa lazima 
ili ujenzi uweze kufanyika mapema.
Akizungumzia madai hayo ya Mbunge 
Dewji, Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Naomi Kapambala alikiri kupata 
nakala ya barua hiyo na kusema kuwa  wamefanya matayarisho yote muhimu 
ikiwa ni pamoja na kufuatilia Airtel makao makuu juu ya suala hilo.
Aidha Kapambala amesema kuwa kamati 
ya siasa imemaliza kazi na kupeleka baraza la wadhamini, na 
kinachosubiriwa na baraza kukaa ili kutoka majibu.
“Mi namshangaa ni kwa nini yeye 
mwenyewe Dewji hajafika hapa ofisini na kupata ufafanuzi juu ya hili 
matokeo yake analeta nakala ya barua kwetu, akamwulize katibu Mkuu 
ambaye amemwandikia hii barua.” Alisema Kapambala
Hata wakati katibu mkuu alipokuja 
hapa tulimweleza juu ya hilo , yeye kama anaonaje  ni vyema akafika 
ofisini ili kujua inachoendelea.
Sehemu ya jukwaa la uwanja wa Namfua linalotumiwa na washabiki likiwa linaonekana kuchakaa.
Aidha Kapambala amesema Katibu mkuu 
msaidizi yuko jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine 
wamemwagiza kupitia baraza la wadhamini wa CCM ili kujua hatma ya suala 
hilo.
Pia Kapambala amesema pia ofisi yake
 imekwishatoa notisi kwa wafanyabiashara mbalimbali kuondoka kwenye eneo
 la uwanja ili kupisha ukarabati huo.
Mwenyekiti wa SIREFA Baltazari 
Kimario alisema anasikitishwa kuona maendeleo ya uwanja huo bado 
haujakamilika na hivyo kuathiri maendeleo ya soka katika mkoa wa 
singida.
Aidha wadau mbalimbali nao wametoa 
masikitiko yao kwa uongozi wa CCM  Mkoa wa singida kuchelewesha mchakato
 huo kwa maslahi binafsi, huku Mbunge akiwa tayari kushughulikia kero 
hiyo.
Uwanja huo hivi sasa umebaki kuwa 
kama eneo maarufu la vijana kuvuta bangi na wengine kujisaidia hovyo 
kwenye vyoo na hivyo kutapakaa kwa vinyesi kila mahali ndani ya uwanja 
huo.
Ujenzi wa Uwanja wa Namfua,ambao 
ulikuwa ukienda sambamba na Jengo la CCM mkoa, ulisimama miaka ya 1990 
na tangu wakati huo uwanja huo umebakia gofu na kugeuka maficho ya 
wahalifu mbalimbali na eneo la choo cha jumuiya.
Baadhi ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida wakipiga picha jengo la makao makuu ya CCM Mkoa wa Singida.
Vijana hawa walikutwa wakivuta bangi kwenye majukwaa ya uwanja wa Namfua.
Hapa ndio makao makuu ya CCM Mkoa wa Singida.(Picha zote na Hillary Shoo).
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
0 comments:
Post a Comment