Mh.
 Dr. Christine Ishengoma Mkuu wa Mkoa wa Iringa akipokea taarifa kuhusu 
mfumo wa taarifa za masoko kutoka TAHA unavyofanya kazi zake kutoka kwa 
Cyrila Antony Afisa wa Masoko
Mkuu
 wa mkoa wa Iringa  Mh. Dr. Christine Ishengoma akisikiliza maelezo 
kutoka kwa Mtaalamu wa kilimo wa TAHA Bw Ringo kuhusu uzalishaji wa zao 
la nyanya 
Elimu ikiendelea kutolewa
 Vitalu na green houses
 Aina Mbalimbali za matunda ambazo zimezalishwa na wakulima kutokana na elimu Bora waliyo ipata kutoka TAHA
 Mwananchi akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa TAHA
 Teknolojia ya umwagiliaji kwa mfumo wa kilimo cha matone ambao pia unaonesha utengenezaji bora wa matuta, nafasi na usafi
Hivi ni  Vitalu vya TAHA na Barton Tanzania
 Vitalu vya mboga na green house kama zinavyoonekana katika picha
 Watangazaji wa Radio Sweet FM ya Mbeya wakishangaa ubora wa karoti ambayo ni daraja la kwanza inapopelekwa sokoni
 Zao la chines
Zao la karoti lililopandwa kwenye vitalu vilivyopo ndani ya viwanja vya Nanenane Mbeya kwenye Banda la TAHA
 Mwananchi akifurahia maelezo kuhusu zao la karoti daraja la kwanza
********************
Wakulima
 na wananchi mkoani Mbeya wameendelea kuneemeka na elimu ya bure ya 
uzalishaji wa mazao ya mboga, viungo na matunda inayotolewa na Asasi ya 
wakulima, wafanyabiashara na watoa huduma ya mazao ya horticulture 
nchini Tanzania (TAHA).
Wakulima
 hao wameneemeka na elimu hiyo inayotolewa na maafisa wa ufundi wa 
kilimo kutoka TAHA kwa ushirikiano na wale wa Barton Tanzania ambao kwa 
pamoja wameweka kambi katika viwanja hivyo ili kuhakikisha jamii ya 
wakulima wa mboga kutoka ukanda wa Nyanda za Juu Kusini wanapata elimu 
ya msingi bora ya uzalishaji wa mboga wenye tija.
"Mpaka
 sasa tumetembelewa na wananchi na wakulima wasiopungua 460 ambao 
wamefika katika banda letu hapa Nanenane kwenye viwanja vya John 
Mwakangale wakitaka kujifunza mbinu na misingi ya awali ya uzalishaji wa
 mazao ya horticulture, hiyo ni ishara njema kwani inaonesha ni kiasi 
gani wananchi  wanatafuta mbinu fasaha inayoweza kuwakwamua kutoka 
katika uzalishaji wa mboga wa kawaida mpaka uzalishaji wa tija 
unaozingatia viwango vya kitaifa na kimataifa" Alisema Likati Thomas 
afisa Mawasiliano kutoka TAHA.
Akifafanua
 zaidi kuhusu elimu ya kilimo cha uzalishaji wa mboga kwenye banda la 
TAHA afisa mawasiliano huyo alisema kuwa wamepanda mazao tofauti katika 
ploti zilizopo kwenye eneo lao ambapo wakulima na wananchi wanaopata 
fursa ya kutembelea eneo hilo ujifunza teknolojia mbalimbali za 
uzalishaji kama vile uzalishaji unaozingatia Mbegu bora zenye tija.
Teknolojia
 nyingine ni pamoja na upandaji mazao unaozingatia nafasi kati ya miche 
na miche, umwagiliaji kwa njia ya matone(drip irrigation) unaozingatia 
uhifadhi wa maji na mazingira pamoja na ulimaji wa matuta yaliyoinuka 
ili kutoa nafasi kwa mizizi ya mimea kupenyeza kwenye udongo ili 
kujitafutia lishe.
Mbali
 na elimu hiyo ya uzalishaji wa mboga, wananchi wa Mbeya wanaotembelea 
banda hilo pia wanapata fursa ya kujifunza elimulishe kutoka kwa 
mtaalamu wa masuala ya lishe wa TAHA Bi. Lawrencia …..ambaye amekuwa 
akiwafundisha wananchi juu ya umuhimu wa ulaji wa mboga na faida zake 
kwa afya ya miili yetu.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment