Home » » HANJE BANARBAS AUKWAA TENA UENYEKITI WA CCM SINGIDA VIJIJINI KWA MIAKA MITANO IJAYO.

HANJE BANARBAS AUKWAA TENA UENYEKITI WA CCM SINGIDA VIJIJINI KWA MIAKA MITANO IJAYO.


Mgombea nafasi ya uenyekiti wa CCM wilaya ya Singida vijijini Hanje Narumba Barnabas akijinadi kuomba kura kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi CCM (hawapo pichani) huku akiwa amebeba biblia mkononi.Hanje alitetea nafasi yake hiyo baada kupata kura 607.
Mwenyekiti mteule wa CCM wilaya ya Singida vijijini Hanje Narumba Barnabas akiwa haamini kama kweli katetea nafasi yake kutokana na upinzani mkali kwenye uchaguzi huo.
Baadhi ya wajumbe 1,200 waliohudhuria mkutano mkuu wa uchaguzi wa CCM wilaya ya Singida vjijini.(Picha na  Nathaniel Limu).
Mkutano mkuu wa uchaguzi CCM wilaya ya Singida vijijini umemchagua tena Hanje Narumba Banarbas, kuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Hanje ametetea kiti chake hicho baada ya kupata kura 607 na kufuatiwa kwa mbali na mpinzani wake wa karibu Mwiru Juma aliyepata kura 480.
Waombaji wengine wa nafasi hiyo ya mwenyekiti  wa wilaya, ni Ngala aliyepata  kura 56 na Sima Luther aliambulia kura 51.
Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii Lazaro Samweli Nyaland alishinda kwa kishindo nafasi ya mjumbe wa halmashauri ya taifa (NEC), baada ya kupata kura 897 kati ya kura 1,157 zilizopigwa.
 Mh. Nyalandu ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Singida Kaskazini, alifuatiwa kwa mbali na Dafi Bulali aliyepata kura 131,huku Manase Saba Saba (102) na Juma kura 27 tu.
Msimamizi wa uchaguzi huo Mosses Matonya, aliwatangaza washindi wa tano wa mkutano mkuu taifa na kura zao kwenye mabano, kuwa Monko (819) na mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi (731).
Aliwataja wengine kuwa ni Amani Nyekele (572), Rehema Majii (554) na Aziza Kiduda (455).
Nafasi hiyo ya wajumbe watano ilikuwa inawaniwa na wajumbe 12.
Matonya ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Manyoni, aliwataja washindi wa nafasi za ujumbe wa halmashauri kuu wilaya kundi la vijana, kuwa ni Manase Sabasaba (705), Jumanne Salum (716), Daud Elias (665) na Hilda Lazaro (666).
Alisema nafasi ya wajumbe wa halmashauri wilaya kupitia kundi la wanawake, zimechukuliwa na Amina Mweri aliyepata kura 1,468, Hilda Lazaro (672), Neema Matiti (696) na Zuena Mohammede (621).
Matonya alisema nafasi za wajumbe wa halmashauri kuu kundi la wazazi, zimechukuliwa na Justin Monko aliyepata kura 646, Edward Yaredi (374), Ilanda (353) na Ramadhani Mangu (292).
Awali mwenyeikiti wa CCM anayemaliza muda wake Joramu Allute, waliwataka wajumbe kuchagua viongozi wenye makazi yao mkoani Singida na si vingionevyo, kwa madai kuwa viongozi hao watawatumikia wananchi kwa muda mwingi zaidi.
Allute anatetea nafasi yake hiyo.
Pia mgombea mwingine wa nafasi ya mwenyekiti CCM mkoa Amani Rai alisema kuwa nyakati za kuongozwa na wazee zimepita na sasa ni nyakati za vijana kuongoza kwa madai wana uwezo wa kukabiliana na upinzani.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa