Home » » SIRUNGONET YAANZA KUENDESHA MIDAHALO

SIRUNGONET YAANZA KUENDESHA MIDAHALO



na Jumbe Ismaily, Singida
MTANDAO wa asasi za kiraia wilaya ya Singida vijijini (SIRUNGONET) umetangaza kuanza kuendesha midahalo ya mikakati ya kupunguza umaskini na kuongeza kipato kwa jamii kwenye jimbo la Singida Kaskazini, Singida Magharibi na Singida Mashariki.
Mratibu wa Sirungonet wilayani hapa, Sombi Sombi, alisema jana kuwa leo wataanza mdahalo katika kijiji cha Itaja, tarafa ya Mgori.
Alisema Oktoba 23, wataendesha mdahalao kijiji cha Puma, kilichoko jimbo la Singida Magharibi kuanzia saa tatu asubuhi ambapo wananchi watapata fursa ya kutoa maoni yao wakati saa sita mchana wananchi wa kijiji cha Dung’unyi katika jimbo la Singida Magharibi watapa nafasi ya kutoa maoni yao pia.
Aidha, mratibu huyo alisema lengo la midahalo hiyo ni kuimarisha mahusiano kati ya wananchi na wabunge au wawakilishi wao.
“Midahalo hii inalenga kutoa fursa ya majadiliano kati ya wabunge, madiwani na watendaji wa serikali ili kuimarisha ari ya ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi katika kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo,” alisema.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa