Home » » MKULIMA WA SINGIDA KIZIMBANI KWA TUHUMA KUMNAJISI MWANAE WA DARASA LA PILI.

MKULIMA WA SINGIDA KIZIMBANI KWA TUHUMA KUMNAJISI MWANAE WA DARASA LA PILI.



Na Nathaniel Limu.
Kijana mmoja mkulima wa kijiji cha Ughandi ‘B’ tarafa ya Mtinko jimbo la Singida kaskazini, amepandishwa kizimbani akituhumiwa kumwingilia kimwili mtoto wake wa kike anayesoma darasa la pili.
Kijana huyo ni Juma Abrahaman na umri wake ni miaka thelathini (30).
Mwendesha mashitaka Geofrey Luhanga amedai mbele ya hakimu wa mahakama ya wilaya ya Singida Flora Ndale, kuwa mnano Septemba 9 mwaka huu majira ya jioni, mshitakiwa Juma kwa makusudi, alimwingilia kimwili mtoto wake wa kike kitendo anachojua wazi kuwa ni kinyume na sheria.
Akifafanua amedai kuwa mshitakiwa alimwita mtoto wake (jina tunalo) chumbani kwake na kisha kumfanyia kitendo hicho cha kinyama.
Wakati mshitakiwa akifanya kitendo hicho mke wake alikuwa jirani akiendelea na shughuli zake za nyumbani.
Mshitakiwa amekana shitaka na yupo ndani hadi oktoba 31 mwaka huu kesi yake itakapotajwa tena.
Mshitakiwa alishindwa kupata mtu wa kumdhamini na hivyo kulazimika kwenda mahabusu gerezani.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa