Home » » Magufuli Ateta Na Makandarasi

Magufuli Ateta Na Makandarasi


 Akizungumza na uongozi wa kampuni ya CHICO (hawapo pichani), Magufuli aliwataka kutekeleza mradi huo kwa kuzingatia makubaliano
 John Magufuli akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya CHICO
 Magufuli akikagua barabara inayokarabatiwa na kampuni ya CHICO kutoka nchini China baada ya kujenga chini ya kiwango mwaka 2008
 Meneja TANROADS mkoa Singida Yustak Kangole akitoa taarifa ya marudio ya ujenzi wa barabara Sekenke-Shelui, km 33.3, kwa waziri
Singida.
Oktoba09,2012.
Makandarasi.....
WIZARA ya Ujenzi imewakumbusha Wakandarasi nchini kujenga barabara zinazolingana na thamani ya fedha, iliyopo kwenye mikataba yao.
Agizo hilo limetolewa leo mkoani Singida na Waziri John Magufuli, wakati anakagua marudio ya ujenzi wa barabara, eneo la mlima Sekenke-Shelui, yenye urefu wa kilomita 33.3.
Amesema serikali imetumia zaidi ya Sh.Bilioni 35, kugharamia ujenzi huo, lakini mkandarasi China Henan International Cooparation Group Co Ltd(CHICO), ilijenga chini ya kiwango.
Aidha ameuagiza uongozi wa kampuni hiyo kuwapatia wafanyakazi wake vifaa vya kufanyia kazi, hasa viatu na gloves kwa ajili ya kuvaa mikononi.
Hata hivyo meneja TANROADS Mkoa Singida, Yustak Kangole amesema barabara hiyo baada ya kukamilika Januari, 2008, ilichukua miezi miwili kuanza kubomoka, kutokana na ujenzi hafifu. 
Kwa mujibu wa meneja mradi wa barabara hiyo, mhandisi Stone Chen, marudio ya ujenzi yanaigharimu kampuni zaidi ya S h.Bilioni kumi. 
Na Elisante John 




0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa