Home » » WANANCHI SINGIDA KUANZA KUTOA MAONI JUU YA KATIBA KUANZIA OKTOBA 17-27, 2012.

WANANCHI SINGIDA KUANZA KUTOA MAONI JUU YA KATIBA KUANZIA OKTOBA 17-27, 2012.



Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya ujio wa tume ya kukusanya maoni ya Katiba kwenye wilaya hiyo.
(Picha na Nathaniel Limu).
Na  Nathaniel Limu.
Tume ya mabadiliko ya katiba, inatarajia kuanza kukusanya maoni ya wananchi wa wilaya ya Singida kuanzia oktoba 17 hadi 27 mwaka huu.
Akitoa taarifa ya ujio wa tume hiyo wilayani humo kwa waandishi wa habari hiyo Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi  amesema  wilaya hiyo yenye halmashauri mbili, tume hiyo itaanza kukusanya maoni kwenye kata kumi za halmashauri ya manispaa ya Singida kuanzia Oktoba 17 hadi 21 mwaka huu.
Amezitaja kata hizo za manispaa kuwa ni wankoko,Unyambwa,Mandewa,Mtipa,Kisaki,Mungumaji,Majengo,Unyambwa,Mughanga na Mtamaa.
Aidha, mkuu wa wilaya amesema kwa upande wa halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini, tume hiyo itaanza kukusanya maoni kuanzia oktoba 22 hadi 27 mwaka huu.
Mlozi ametaja kata zilizochaguliwa kutembelewa na tume hiyo kuwa ni Msisi,Kinyeto,Mtinko,Maghojoa,Mgori,Ngimu,Merya,Ilongero,Maghojoa,Mgori,Ngimu,Merya,Ilongero, Ughandi na Ngamu.
Amesema kila siku tume hiyo itakapo tembelea kata mbili ambapo kata ya kwanza wananchi watatoa maoni yao kuanzia saa tatu asubuhi na kata ya pili shughuli itaanza saa nane mchana.
Alitumia fursa hiyo kutoa wito kwamba wananchi wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao wakati watakapokuwa wanapewa muda wa dakika tano na endapo itashindikana kutumia njia hiyo,basi watumie njia ya kuandika maoni yao kwa maandishi.
Pia amewaonya kwamba wasishawishiwe na mtu au kiongozi katika kutoa maoni yao.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa