Home » » KDU wakamata majangili zaidi ya 600

KDU wakamata majangili zaidi ya 600

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KIKOSI cha Kuzuia Ujangili (KDU)KIKOSI cha Kuzuia Ujangili (KDU) Kanda ya Kati, kimefanikiwa kukamata majangili 692 na meno ya tembo 195 katika Operesheni Tokomeza Ujangili iliyofanyika wilayani Manyoni, Singida kuanzia mwaka 2009 hadi 2012.
Kaimu Meneja wa Hifadhi ya Pori la Akiba la Rungwa, Batholomeo Mganga, alisema hayo wakati wa kumkabidhi baiskeli ya miguu mitatu mlemavu, Yohana Pangarasi, mwanakijiji wa Imalampaka, Manyoni.
Mganga alisema katika kipindi hicho tembo 168 wenye uzito wa kilo 166 waliuawa na majangili hao kinyume cha sheria.
Hata hivyo Kaimu Meneja wa KDU alisema mwaka 2009 licha ya kukamatwa kwa majangili 116, tembo 16 waliuawa wakati mwaka 2010 majangili 172 walikamatwa wakiwa na meno ya tembo manne yaliyokuwa na uzito wa kilo 23.5
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa