Katibu
 wa chama cha waandishi wanawake (Women in Media Organization - WMO) 
tawi la mkoa wa Singida, Awila Silla, akitoa taarifa yake ya msaada wa 
mizinga 80 kwa vikundi vinne vya wafuga nuki wanawake kutoka wilaya ya 
Singida na Ikungi.
Mkuu
 wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akizungumza kwenye hafla ya 
kukabidhi msaada wa mizinga ya nyuki kwa vikundi vinne vya Wanawake 
wafuga Nyuki.Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi na kulia 
ni mwenyekiti wa WMO Evarista Lucas.
Mkuu
 wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone (wa pili kulia) akikabidhi mzinga 
wa Nyuki kwa wawakilishi wa vikundi vinne vya wafuga Nyuki wa wilaya ya 
Singida na Ikungi.Wa kwanza kulia ni Afisa Maliasili mkoa wa 
Singida,Charles Kidua.
Mkuu
 wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, (wa pili kulia walioketi) akiwa 
kwenye picha ya pamoja na wanakikundi wa ufugaji nyuki kutoka wilaya ya 
Singida na Ikungi.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa WMO Evarista 
Lucas.Kushoto ni afisa maliasili mkoa Charles Kidua na anayefuata ni 
mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
CHAMA
 cha Waandishi wa Wanawake (Women in Media Organization – WMO) mkoani 
Singida kimetoa msaada wa miziga 80 ya nyuki ya kisasa, kwa vikundi vine
 vya wanawake wa halmashauri ya Singida na Ikungi.
Mizinga hiyo ya kisasa iliyotengenezwa na SIDO ndogo mjini hapa, inakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi.
Hayo
 yamesemwa hivi karibuni na Katibu wa WMO mkoani Singida, Awila Sill 
wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mizinga hiyo ya kisasa 
iliyofanyika kwenye viwanja vya SIDO mjini Singida.
Amesema
 vikundi hivyo ni kutoka vijiji vya Masweya na Muhintiri vya wilaya ya 
Ikungi na Ilongero na Nduamughanga vya halamashauri ya wilaya ya 
Singida.
Awila
 ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi na the citizen 
mkoani hapa, alisema mizinga hiyo kila moja una uwezo wa kutoa/kuzalisha
 lita 20 na bei ya lita moja kwa sasa ni shilingi 10,000.
“Wanakikundi
 wote,tumeishawapatia mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki.Kwa hiyo 
tunayoimani kuwa mbele ya safari,wanakikundi hawa watanufaika na msaada 
huu na kwa vyo vyote,watajikomboa kiuchumi”,amesema Awila.
Katika
 hatua  nyingine, Katibu huyo alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali 
kupitia wizara ya maliasili na utalii kitengo cha mfuko wa misitu nchini
 kwa kukipatia WMO ruzuku ya zaidi ya shilingi 14.4 milioni.
Kwa
 upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo, mkuu wa mkoa wa Singia, Dk. 
Parseko Vicent Kone, ameziagiza halmashauri za wilaya na manispaa, 
kuongeza juhudi katika kuendelea kuibua vikundi vingi zaidi vya ufugaji 
nyuki.
Aidha,
 ameziagiza kuwaondoa mara moja wavamizi wa misitu na hasa kwenye misitu
 ya vijiji vya Mgori, Minyughe, Mlilii, Sekenke/Tulya, Wembere, Chaya na
 maeneo mengine yaliyoharibiwa.
“Halmashauri
 mnalo jukumu la kuzuia ukataji miti ya asili kwa ajili ya kukaushia 
tumbaku, wakulima wa tumbaku wanapaswa kupanda miti kwa ajili ya 
matumizi yao”,amesema Dk.Kone.
2 comments:
GOOD TRY
GOOD TRY
Post a Comment