Home » » Chama cha waandishi Wanawake chatoa msaada wa Mizinga 80 ya Nyuki

Chama cha waandishi Wanawake chatoa msaada wa Mizinga 80 ya Nyuki

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

DSC07053
Katibu wa chama cha waandishi wanawake (Women in Media Organization - WMO) tawi la mkoa wa Singida, Awila Silla, akitoa taarifa yake ya msaada wa mizinga 80 kwa vikundi vinne vya wafuga nuki wanawake kutoka wilaya ya Singida na Ikungi.
 
DSC07075
 
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa mizinga ya nyuki kwa vikundi vinne vya Wanawake wafuga Nyuki.Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi na kulia ni mwenyekiti wa WMO Evarista Lucas.
DSC07082
 
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone (wa pili kulia) akikabidhi mzinga wa Nyuki kwa wawakilishi wa vikundi vinne vya wafuga Nyuki wa wilaya ya Singida na Ikungi.Wa kwanza kulia ni Afisa Maliasili mkoa wa Singida,Charles Kidua.
DSC07087
 
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, (wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na wanakikundi wa ufugaji nyuki kutoka wilaya ya Singida na Ikungi.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa WMO Evarista Lucas.Kushoto ni afisa maliasili mkoa Charles Kidua na anayefuata ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
CHAMA cha Waandishi wa Wanawake (Women in Media Organization – WMO) mkoani Singida kimetoa msaada wa miziga 80 ya nyuki ya kisasa, kwa vikundi vine vya wanawake wa halmashauri ya Singida na Ikungi.
Mizinga hiyo ya kisasa iliyotengenezwa na SIDO ndogo mjini hapa, inakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi.
Hayo yamesemwa hivi karibuni na Katibu wa WMO mkoani Singida, Awila Sill wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mizinga hiyo ya kisasa iliyofanyika kwenye viwanja vya SIDO mjini Singida.
Amesema vikundi hivyo ni kutoka vijiji vya Masweya na Muhintiri vya wilaya ya Ikungi na Ilongero na Nduamughanga vya halamashauri ya wilaya ya Singida.
Awila ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi na the citizen mkoani hapa, alisema mizinga hiyo kila moja una uwezo wa kutoa/kuzalisha lita 20 na bei ya lita moja kwa sasa ni shilingi 10,000.
“Wanakikundi wote,tumeishawapatia mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki.Kwa hiyo tunayoimani kuwa mbele ya safari,wanakikundi hawa watanufaika na msaada huu na kwa vyo vyote,watajikomboa kiuchumi”,amesema Awila.
Katika hatua  nyingine, Katibu huyo alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii kitengo cha mfuko wa misitu nchini kwa kukipatia WMO ruzuku ya zaidi ya shilingi 14.4 milioni.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo, mkuu wa mkoa wa Singia, Dk. Parseko Vicent Kone, ameziagiza halmashauri za wilaya na manispaa, kuongeza juhudi katika kuendelea kuibua vikundi vingi zaidi vya ufugaji nyuki.
Aidha, ameziagiza kuwaondoa mara moja wavamizi wa misitu na hasa kwenye misitu ya vijiji vya Mgori, Minyughe, Mlilii, Sekenke/Tulya, Wembere, Chaya na maeneo mengine yaliyoharibiwa.
“Halmashauri mnalo jukumu la kuzuia ukataji miti ya asili kwa ajili ya kukaushia tumbaku, wakulima wa tumbaku wanapaswa kupanda miti kwa ajili ya matumizi yao”,amesema Dk.Kone.

2 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa