Kaimu
 meya mstahiki wa manispaa ya Singida, Hassan Mkata akizungumza kwenye 
kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Singida 
kilichofanyika mkoani Singida.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya 
Singida. Robert Mahili na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM manispaa ya 
Singida,Hamisi Nguli.
Diwani
 wa kata ya Unyamikumbi,Mosses Ikaku, akichangia hoja katika kikao cha 
baraza la madiwani wa manispaa ya Singida kilichofanyika mjini Singida.
Afisa
  Ardhi manispaa ya Singida, Angelus John  Camara,akitoa ufafanuzi juu 
ya sheria ya Ardhi mbele ya kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika 
mkoani Singida.
Baadhi
 ya madiwani wa manispaa ya Singida waliohudhuria kikao cha kawaida cha 
baraza la madiwani kilichofanyika mjini Singida.(Picha na Nathaniel 
limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
KUTOKANA
 na uhaba mkubwa wa watumishi wa sekta ya afya katika vituo mbalimbali 
vya afya vikiwemo zahanati,serikali imeshauriwa kuajiri waganga wa jadi 
ili kupunguza uhaba huo.
Ushauri
 huo wa bure,umetolewa hivi karibuni na Diwani wa kata ya Unyambwa (CCM)
 Manispaa ya Singida,Shaban Satu wakati akichangia hoja ya diwani wa 
kata ya Unyamikumbi,Mosses Ikaku ambaye alidai zahanati ya kata yake 
imekuwa na mhudumu moja tu kwa kipindi kirefu.
Amesema uzoefu unaonyesha kuwa uhaba wa wahudumu wa afya una athari nyingi ikiwemo ya utoaji wa huduma usiokidhi mahitaji.
“Diwani
 mwenzetu ametueleza kwamba kwa muda mrefu amefikisha tatizo la uhaba wa
 wahudumu katika ngazi husika mara nyingi,lakini juhudi zake hazijazaqa 
matunda hadi sasa”,amesema.
Amesema
 endapo serikali imeshindwa kulitafutia ufumbuzi wa kudumu tatizo 
hilo,basi ni bora ikatoa nafasi kwa waganga wa jadi kuziba mapungufu 
hayo”,alifafanua.
Katika hatua nyingine,imedaiwa kuwa shule ya msingi ya kijiji cha Mwankoko,inakabiliwa na uhaba wa madawati 316.
Kaimu
 Mkurugenzi wa manispaa hiyo,Robert Mahili aliiomba serikali ya kijiji 
hicho kuongeza juhudi zaidi kuhamasisha wananchi kuchangia ununuzi wa 
madawati.
Amesema
 pia juhudi zilifanyika za za kuzishawishi benki ya NBC,CRDB,NMB na 
CIP,ili ziweze kusaidia kuondoa uhaba huo mkubwa wa madawati.
Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi,Mahili,manispaa hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu 298.
0 comments:
Post a Comment