Home » » Serikali yashauriwa kuajiri Waganga wa Jadi kupunguza uhaba wa watumishi wa Afya

Serikali yashauriwa kuajiri Waganga wa Jadi kupunguza uhaba wa watumishi wa Afya

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

DSC06762
Kaimu meya mstahiki wa manispaa ya Singida, Hassan Mkata akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Singida kilichofanyika mkoani Singida.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Singida. Robert Mahili na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM manispaa ya Singida,Hamisi Nguli.
DSC06736
Diwani wa kata ya Unyamikumbi,Mosses Ikaku, akichangia hoja katika kikao cha baraza la madiwani wa manispaa ya Singida kilichofanyika mjini Singida.
DSC06751
Afisa  Ardhi manispaa ya Singida, Angelus John  Camara,akitoa ufafanuzi juu ya sheria ya Ardhi mbele ya kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika mkoani Singida.
DSC06757
Baadhi ya madiwani wa manispaa ya Singida waliohudhuria kikao cha kawaida cha baraza la madiwani kilichofanyika mjini Singida.(Picha na Nathaniel limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
KUTOKANA na uhaba mkubwa wa watumishi wa sekta ya afya katika vituo mbalimbali vya afya vikiwemo zahanati,serikali imeshauriwa kuajiri waganga wa jadi ili kupunguza uhaba huo.
Ushauri huo wa bure,umetolewa hivi karibuni na Diwani wa kata ya Unyambwa (CCM) Manispaa ya Singida,Shaban Satu wakati akichangia hoja ya diwani wa kata ya Unyamikumbi,Mosses Ikaku ambaye alidai zahanati ya kata yake imekuwa na mhudumu moja tu kwa kipindi kirefu.
Amesema uzoefu unaonyesha kuwa uhaba wa wahudumu wa afya una athari nyingi ikiwemo ya utoaji wa huduma usiokidhi mahitaji.
“Diwani mwenzetu ametueleza kwamba kwa muda mrefu amefikisha tatizo la uhaba wa wahudumu katika ngazi husika mara nyingi,lakini juhudi zake hazijazaqa matunda hadi sasa”,amesema.
Amesema endapo serikali imeshindwa kulitafutia ufumbuzi wa kudumu tatizo hilo,basi ni bora ikatoa nafasi kwa waganga wa jadi kuziba mapungufu hayo”,alifafanua.
Katika hatua nyingine,imedaiwa kuwa shule ya msingi ya kijiji cha Mwankoko,inakabiliwa na uhaba wa madawati 316.
Kaimu Mkurugenzi wa manispaa hiyo,Robert Mahili aliiomba serikali ya kijiji hicho kuongeza juhudi zaidi kuhamasisha wananchi kuchangia ununuzi wa madawati.
Amesema pia juhudi zilifanyika za za kuzishawishi benki ya NBC,CRDB,NMB na CIP,ili ziweze kusaidia kuondoa uhaba huo mkubwa wa madawati.
Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi,Mahili,manispaa hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu 298.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa