Home » » ABIRIA WAKWAMA SINGIDA

ABIRIA WAKWAMA SINGIDA

ABIRIA waliokuwa wanasafiri  kutoka Dodoma kuelekea  mikoa  ya kanda ziwa,  magharibi  na  nchi jirani,  leo asubuhi wamekwama kwa zaidi ya saa nne  katika eneo la Kijiji cha Kisaki umbali wa Kilomita 10  kabla ya kufika Singida mjini baada ya madereva wa malori kufunga barabara .

Zaidi ya malori 300 yaliegeshwa barabarani  kuanzia  saa 12 hadi saa 4 asubuhi, kuzuia  magari mengine yasipite ili kulishinikiza jeshi la polisi kudhibiti uhalifu wa mara kwa mara katika eneo hilo baada ya wenzao wawili kutekwa na majambazi, kujeruhiwa kisha kuporwa  fedha  na mali nyingine.

Madereva hao wamesema wamefikia uamuzi wa kufunga barabara ili kuwasilisha hisia zao kwa mamlaka  husika baada ya eneo  hilo na utekaji magari mara.
Wamesema mbali na kuporwa fedha na mali nyingine, pia wamekuwa akijeruhiwa kwa mapanga, pinde na silaha za moto kiasi cha kuhatarisha maisha yao lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.

Madereva hao wamekubali kuendelea na safari  baada  ya Naibu Waziri wa Ushiriano wa Afrika   Mashariki Abdulla Juma Abdull aliyekuwa miongoni mwa watu walikwama eneo hilo,  kuahidi kuifikisha kero hiyo kwa mamlaka husika na ufumbufu wa kudumu kutafutwa haraka iwezekanavyo.

Kamanda wa polisi mkoa  wa Singida Geofrey Kamwela amesema polisi wanaendelea  na msako mkali dhidi ya watu waliofanya utekaji huo wa magari na kupora  madereva fedha pamoja na kuwajeruhi.


Hata  hivyo  ametoa wito  kwa wadau wote kushirikiana  kudhibiti uhalifu  badala ya  kufunga barabara na kuwategemea polisi  peeke ambao ni wachache na hawawezi kuwepo kila mahali penye uhalifu.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa