Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela.
Na Nathaniel Limu, Singida
JESHI
 la Polisi mkoa wa Singida linamshikilia Mariamu Songeraeli (32) mkulima
 mkazi wa kijiji cha Nselembwe wilaya ya Iramba kwa tuhuma ya kumiliki 
madawa ya kulevya aina ya bhangi misokoto 88 yenye uzito wa gramu 44.
Kamanda
 wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela amesema 
mtuhumiwa Mariamu amekamatwa juzi saa 11.30 jioni nyumbani kwake katika 
kijiji cha Nselembwe kata ya Shelui wilaya ya Iramba.
Amesema
 askari polisi waliokuwa kwenye doria siku ya tukio,walipata taarifa 
kutoka kwa raia wema kwamba mtuhumiwa Mariamu anajihusisha na biashara 
haramu ya kununua na kuuza bhangi.
Kamwela
 amesema askari hao waliweza kwenda nyumbani kwa mtuhumiwa na kuipekua 
na kisha kuikuta misokoto hiyo ya bhangi ikiwa chumbani kwake,imefichwa 
kwenye mfuko wa rambo.
“Tunamshikilia
 mtuhumiwa kwa uchunguzi zaidi,ili kujua ni wapi anakoitoa bhangi hiyo 
na watu anaoshirikiana nao katika bishara hiyo haramu,baada ya uchunguzi
 huo kukamilika,atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma 
inayomkabili”,amesema.
Aidha,Kamwela
 ametumia fursa hiyo kuwashukuru na kuwapongeza raia wema kwa kutoa 
taarifa sahihi za uhalifu na wahalifu,na kuwaomba waendelee na moyo huo 
huo,kwa madai kwamba suala la usalama ni la wananchi wote kwa ujumla.
Chanzo Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment