Mkuu
 wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akipasua jiwe kubwa ili liweze 
kupandishwa kwenye lori kwa lengo kuondolewa kando kando ya barabara kuu
 ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida. Mawe 
hayo makubwa kwa kipindi kirefu yametumiwa na watu wanaodhaniwa ni 
majamabazi watekaji wa malori na kupora mali na fedha.
Mkazi
 wa kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida, Juma akipasua jiwe kubwa 
lililokuwa likitumiwa na majambazi kwa ajili ya kuteka magari na kisha 
kupora abiria.
Askari
 Polisi, Jeshi na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kisaki manispaa ya 
Singida,wakipandisha jiwe kubwa kwenye lori. Zoezi hilo la kuondoa mawe 
makubwa kando kando ya barabara kuu ya Singida yaliyokuwa yakitumiwa na 
watu wanaodhaniwa ni majambazi katika kuteka magari na kupora abiria. 
Mawe hayo mwishoni mwa mwaka jana yalitumika kuteka gari la chuo cha SUA
 Morogoro na kisha maiti ndani ya sanduku. 
 Mo Blog
0 comments:
Post a Comment