Home » » Mama mlemavu wa ngozi ashikiliwa kwa kumuua mwanawe

Mama mlemavu wa ngozi ashikiliwa kwa kumuua mwanawe

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela
 
Polisi mkoani Singida inawashikilia wanawake wawili akiwamo mlemavu wa ngozi (albino), kwa mauaji ya mtoto Daud Richard (2.5), kwa imani za kishirikiana.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela (pichani), alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 1:30 asubuhi katika kijiji cha Nkalankala tarafa ya Nduguti, wilaya Mkalama.
 
Aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni bibi wa mtoto huyo, Neema Paulo (35) na mama wa marehemu, Hidaya Omari (20).
 
Alisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kabla ya kufikwa na mauti, mtoto huyo alinyongwa shingoni, kuchunwa ngozi sehemu zake za siri na wauaji kutoweka nazo, kisha mwili wake kutumbukizwa ndani ya kisima kilichokuwa na maji.
 
Kamwela alisema kuwa mwili wa mtoto huyo baadaye ulionekana baada ya kuelea juu ya maji na wananchi kutoa taarifa polisi.
 
"Mauaji haya yanahusishwa na imani ya kishirikina kutokana na kuchunwa ngozi na kunyofolewa sehemu za siri...lazima pia tuwashikilie wanawake hawa, walikuwa wapi wakati mtoto kama huyu mdogo anatoweka nyumbani!, hata ndugu wengine pia watahojiwa," alisema Kamwela.
 
Kufuatia tukio hilo Kamwela alisema kuwa mama wa mtoto huyo ambaye ni mlemavu wa ngozi na bibi wa marehemu kwa pamoja watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
 
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa