Home » » 'NILIANZA KAZI NIKAMKUTA AMELAZWA ,SASA NAKARIBIA KUSTAFU NITAMWACHA'

'NILIANZA KAZI NIKAMKUTA AMELAZWA ,SASA NAKARIBIA KUSTAFU NITAMWACHA'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Muuguzi wa Wodi Namba Nne katika Hospitali ya Mkoa wa Singida, Belta Lyamboko amesema alipoanza kazi katika hospitali hiyo mwanzoni mwa mwaka 1981, alimkuta Mzee Abdi Lanjuu (75) na sasa anajiandaa kustaafu akiamini atamwacha mzee huyo hospitalini.
Mzee Lanjuu amelazwa hospitalini hapo kwa miaka 43 sasa baada ya kupata ajali ya lori mwaka 1971, alipokuwa mtumishi wa iliyokuwa Mamlaka ya Pamba Tanzania (TCA), Mkoa wa Mwanza.
Kuishi kwake hospitalini hapo kwa miaka mingi, kumechangiwa na kutokuwa na ndugu wala rafiki wa kumhudumia. “Wakati ninaanza kazi nikiwa kijana, Mzee Abdi alikuwa na nguvu na alikuwa akitembelea kiti cha magurudumu, lakini katika miaka mitatu au zaidi hali yake imekuwa mbaya na hawezi kutembea hata kwa kutumia kiti chake cha magurudumu. Kila kitu pamoja na kula anafanya akiwa amelala kitandani na anasaidiwa na wauguzi... tumeshamzoea na ametuzoea na sasa tunaishi naye kama ndugu,” alisema.
Alisema kuwa tangu aanze kumwona mzee huyo hospitalini hapo, hakuwahi kuwaona ndugu wala rafiki wanaokuja kumtembelea au kumjulia hali.
“Kutokana na hali hiyo na kukaa naye kwa miaka 43 sasa, kila mmoja anamwona ni ndugu, sasa utamfanya nini na yuko hapa...tunaishi naye, tunampatia misaada midogomidogo ya kumwezesha kupata mlo, kinachopatikana tunampatia na tunaendelea kumsaidia, hatutachoka,” alisema.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa