Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Muuguzi wa Wodi Namba Nne katika Hospitali ya Mkoa wa Singida, 
Belta Lyamboko amesema alipoanza kazi katika hospitali hiyo mwanzoni mwa
 mwaka 1981, alimkuta Mzee Abdi Lanjuu (75) na sasa anajiandaa kustaafu 
akiamini atamwacha mzee huyo hospitalini.
                
              
Mzee Lanjuu amelazwa hospitalini hapo kwa miaka 43
 sasa baada ya kupata ajali ya lori mwaka 1971, alipokuwa mtumishi wa 
iliyokuwa Mamlaka ya Pamba Tanzania (TCA), Mkoa wa Mwanza.
Kuishi kwake hospitalini hapo kwa miaka mingi, 
kumechangiwa na kutokuwa na ndugu wala rafiki wa kumhudumia. “Wakati 
ninaanza kazi nikiwa kijana, Mzee Abdi alikuwa na nguvu na alikuwa 
akitembelea kiti cha magurudumu, lakini katika miaka mitatu au zaidi 
hali yake imekuwa mbaya na hawezi kutembea hata kwa kutumia kiti chake 
cha magurudumu. Kila kitu pamoja na kula anafanya akiwa amelala 
kitandani na anasaidiwa na wauguzi... tumeshamzoea na ametuzoea na sasa 
tunaishi naye kama ndugu,” alisema.
Alisema kuwa tangu aanze kumwona mzee huyo 
hospitalini hapo, hakuwahi kuwaona ndugu wala rafiki wanaokuja 
kumtembelea au kumjulia hali.
“Kutokana na hali hiyo na kukaa naye kwa miaka 43 
sasa, kila mmoja anamwona ni ndugu, sasa utamfanya nini na yuko 
hapa...tunaishi naye, tunampatia misaada midogomidogo ya kumwezesha 
kupata mlo, kinachopatikana tunampatia na tunaendelea kumsaidia, 
hatutachoka,” alisema.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment