Home » » KINANA AWASILI SINGIDA

KINANA AWASILI SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini Ndugu Lazaro Nyalandu katika kijiji cha Kaskazi mkoani Singida,Katibu Mkuu atakuwa kwenye ziara ya siku nane mkoani Singida.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaidiana na mafundi kupandish bati wakati wa ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari Mgando,Singida
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na viongozi wa CCM mkoa wa Singida na Kundi la akina mama wajasiriamali wa Itagata kuelekea kwenye mkutano wa hadhara  baada ya kufungua shina la akina mama hao wa Itagata,Singida.
 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa bwawa la maji la Itagata,Singida.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Itigi mkoani Singida .
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Itigi na kuwaambia  CCM ipo imara na kuwaambia wananchi hao muungano  wa vyama vya siasa unaofahamika  kama UKAWA ndio utahitimisha maisha ya baadhi ya vyama vya siasa nchini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma barua ya wakazi wa Tura ambao wanahitaji kujengewa kivuko kwenye reli ili kuwasaidia kwenda kuchota maji bila matatizo kwani kwa sasa wanapata tabu,Katibu Mkuu alisimama Tura kuwasalimu wananchi na kisha kuendelea na safari kuelekea Singida.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa