Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Uongozi wa Kampuni ya Mabasi ya Sumry ya Sumbawanga, Rukwa 
umetoa ubani wa Sh5.5 milioni kwa familia za ndugu na jamaa waliofariki 
dunia kutokana na ajali ya moja ya mabasi yake iliyotokea Aprili 28 
katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi, Singida.
                
              
Katika ajali hiyo, watu 19 wakiwamo polisi wanne, 
walifariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo lililokuwa likitoka 
Kigoma kwenda Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza 
iliyolihusisha lori na mwendesha baiskeli ambaye alipoteza maisha katika
 eneo hilo baada ya kugongwa na lori hilo. Wakazi hao waliogongwa 
walikuwa wamekusanyika kushuhudia ajali hiyo.
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hipoliti Daniel 
Kholani alisema rambirambi hiyo ilikabidhiwa kwa Serikali ya Kijiji na 
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone ambaye naye alichangia 
Sh100,000.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, 
Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio 
jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.
“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea 
kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole 
kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho 
(leo), kuwaombea ndugu zetu.”
Kholani alisema wakazi wa kijiji hicho, Mussa 
Mohammed, Suku Abdallah na Ayubu Ramadhani bado wamelazwa hospitalini 
wakiendelea kutibiwa majeraha waliyoyapata kwenye ajali ya basi hilo 
ambalo bado lipo Kituo cha Polisi Ikungi.Uongozi wa Kampuni ya Mabasi ya Sumry ya Sumbawanga, Rukwa 
umetoa ubani wa Sh5.5 milioni kwa familia za ndugu na jamaa waliofariki 
dunia kutokana na ajali ya moja ya mabasi yake iliyotokea Aprili 28 
katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi, Singida.
                
              
Katika ajali hiyo, watu 19 wakiwamo polisi wanne, 
walifariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo lililokuwa likitoka 
Kigoma kwenda Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza 
iliyolihusisha lori na mwendesha baiskeli ambaye alipoteza maisha katika
 eneo hilo baada ya kugongwa na lori hilo. Wakazi hao waliogongwa 
walikuwa wamekusanyika kushuhudia ajali hiyo.
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hipoliti Daniel 
Kholani alisema rambirambi hiyo ilikabidhiwa kwa Serikali ya Kijiji na 
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone ambaye naye alichangia 
Sh100,000.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, 
Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio 
jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.
“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea 
kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole 
kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho 
(leo), kuwaombea ndugu zetu.”
Kholani alisema wakazi wa kijiji hicho, Mussa 
Mohammed, Suku Abdallah na Ayubu Ramadhani bado wamelazwa hospitalini 
wakiendelea kutibiwa majeraha waliyoyapata kwenye ajali ya basi hilo 
ambalo bado lipo Kituo cha Polisi Ikungi.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment