Home » » SUMRY YATOA UBANI WA SH.5.5M AJALI SINGIDA

SUMRY YATOA UBANI WA SH.5.5M AJALI SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho (leo), kuwaombea ndugu zetu

Uongozi wa Kampuni ya Mabasi ya Sumry ya Sumbawanga, Rukwa umetoa ubani wa Sh5.5 milioni kwa familia za ndugu na jamaa waliofariki dunia kutokana na ajali ya moja ya mabasi yake iliyotokea Aprili 28 katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi, Singida.
Katika ajali hiyo, watu 19 wakiwamo polisi wanne, walifariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo lililokuwa likitoka Kigoma kwenda Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza iliyolihusisha lori na mwendesha baiskeli ambaye alipoteza maisha katika eneo hilo baada ya kugongwa na lori hilo. Wakazi hao waliogongwa walikuwa wamekusanyika kushuhudia ajali hiyo.
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hipoliti Daniel Kholani alisema rambirambi hiyo ilikabidhiwa kwa Serikali ya Kijiji na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone ambaye naye alichangia Sh100,000.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.
“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho (leo), kuwaombea ndugu zetu.”
Kholani alisema wakazi wa kijiji hicho, Mussa Mohammed, Suku Abdallah na Ayubu Ramadhani bado wamelazwa hospitalini wakiendelea kutibiwa majeraha waliyoyapata kwenye ajali ya basi hilo ambalo bado lipo Kituo cha Polisi Ikungi.Uongozi wa Kampuni ya Mabasi ya Sumry ya Sumbawanga, Rukwa umetoa ubani wa Sh5.5 milioni kwa familia za ndugu na jamaa waliofariki dunia kutokana na ajali ya moja ya mabasi yake iliyotokea Aprili 28 katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi, Singida.
Katika ajali hiyo, watu 19 wakiwamo polisi wanne, walifariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo lililokuwa likitoka Kigoma kwenda Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza iliyolihusisha lori na mwendesha baiskeli ambaye alipoteza maisha katika eneo hilo baada ya kugongwa na lori hilo. Wakazi hao waliogongwa walikuwa wamekusanyika kushuhudia ajali hiyo.
Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Hipoliti Daniel Kholani alisema rambirambi hiyo ilikabidhiwa kwa Serikali ya Kijiji na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone ambaye naye alichangia Sh100,000.
Kholani alisema pia Mbunge wa Singida Magharibi, Mohamed Missanga ametoa Sh600,000 na wakazi wa Tarafa ya Ihanja waishio jijini Dar es Salaam pia wamechanga Sh600,000.
“Tangu kutokea kwa ajali hiyo kijiji kimeendelea kupata idadi kubwa ya wageni kutoka sehemu mbalimbali kuja kutoa pole kwa wafiwa. Tunatarajia kufanya sala maalumu kwenye eneo la tukio kesho (leo), kuwaombea ndugu zetu.”
Kholani alisema wakazi wa kijiji hicho, Mussa Mohammed, Suku Abdallah na Ayubu Ramadhani bado wamelazwa hospitalini wakiendelea kutibiwa majeraha waliyoyapata kwenye ajali ya basi hilo ambalo bado lipo Kituo cha Polisi Ikungi.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa