Mzee
 Abdi Nkhambi Lanjui (75) akiwa wodi namba nne katika hospitali ya mkoa 
mjini Singida. Mzee Lanjui mzaliwa wa kijiji cha Mhintiri tarafa ya 
Ihanja, aliyekuwa dereva wa kampuni ya mamlaka ya Pamba Mwanza, alipata 
ajali katikati ya mwaka 1968 na kulazwa katika hospitali ya Sekoture 
Mwanza na baadaye mwishoni mwa mwaka 1970,alihamishiwa hospitali ya mkoa
 wa Singida, ambako anaishi hadi sasa. Ajali hiyo ilisababisha kukatika 
mawasiliano kati ya kuanzia kiunoni na kushuka chini ambako kumepooza na
 sasa kuna vidonda na sehemu ya mwili juu ya kiuno, bado inafanya 
kazi.(Picha na  Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
MZEE
 Abdi Nkhambi Lanjui (75) ambaye ameishi wodini kwa miaka 45 sasa 
ameiomba serikali,Asasi na jamii kwa ujumla kumsaidia huduma ya chakula 
kwa madai kwamba hana ndugu wa kumsaidia huduma hiyo.
Akizungumza
 na MOblog hivi karibuni, Mzee Abdi ambaye kwa sasa hawezi kabisa 
kunyanyuka kitandani amesema kuwa kwa miaka mingi uongozi wa hospitali 
ya mkoa umemhudumia vizuri chakula cha kutosha.
 Akifafanua
 amesema baada ya hospitali hiyo kusitisha huduma ya chakula kwa 
wagonjwa amekuwa omba omba na maisha yake yamebaki ya mlo moja kwa siku.
 “Kwa
 vile siwezi kunyanyuka kitandani na sina ndugu ye yote nimekuwa 
nikiwaomba msaada manesi na watumishi wengine wa hospitani hapa na 
nashukuru sana hawaniangushi wamekuwa wakinisaidia bila kuchoka na 
wananiwezesha kupata angalau mlo wa siku moja”,amesema.
Mzee
 Abdi pia ametumia fursa hiyo kuomba msaada wa fedha na msindikizaji kwa
 ajili ya kwenda hospitali ya KCMC Moshi mkoa wa Kilimanjaro ili 
akapatiwe huduma ya matibabu.
 “Sababu
 ya mimi kugeuza wodi kuwa makazi yangu ya kudumu ni kutokana na ajali 
iliyosababisha kuanzia kiunoni hadi kwenye nyayo za miguuni,kupooza Kwa 
sababu hivi sasa sinyanyuki kitandani kumepelekea nipate vidoda kuanzia 
makalioni hadi kwenye miguu kwa ujumla kwa sasa naishi maisha magumu 
mno”amesema Mzee Abdi.
Mzee Abdi amelazwa wodi namba nne katika hospitali ya mkoa mjini hapa toka januari mosi mwaka 1971.
Awali
 alilazwa katika hospitali ya Sekoture ya jijini Mwanza kuanzia mwaka 
1969 baada ya kupata ajali ya lori alilokuwa akiliendesha kupasuka tairi
 la mbele.
Amesema
 akiwa hospitali ya Sekoture mwishoni mwa mwaka 1970 hali yake 
ilibadilika na kuwa mbaya na ndipo alipomwomba mwajiri wake mamlaka ya 
pamba imrudishe nyumbani katika kijiji cha Mhintiri tarafa ya Ihanja 
wilaya ya Ikungi ili akasubiri kifo chake.
Hata
 hivyo,amesema uongozi wa mamlaka ya pamba ulikataa kumpeleka kijijini 
kwao na badala yake walimkabidhi katika hospitali ya mkoa wa Singida 
mapema mwaka 1971.
Mzee
 Abdi amesema aliondoka nyumbani kwao Mhintiri mwaka 1962 na kwenda 
Mwanza mjini kusaka maisha bora alijifunza udereva na kisha kufanikiwa 
kuajiriwa na mamalaka ya pamba mwaka 1968.Wakati akiondoka kwao 
alimwacha baba,mama na kaka yake mkubwa.
Toka
 alazwe hospitalini,wazazi wake na ndugu yake pekee walikuwa tayari 
wamefariki dunia kwao walizaliwa watoto wawili tu wa kiume.
0 comments:
Post a Comment