Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Rais mstaafu, Benjamin Mkapa akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk 
Parseko Kone kwenye viwanja vya zahanati ya Kijiji cha Senenemfuru, 
wilaya ya Singida kuzindua nyumba za watumishi 
zilizojengwa na Taasisi 
ya Benjamin Mkapa. 
Rais mstaafu, Benjamin Mkapa amewataka Watanzania kuwa 
waangalifu ili mchakato wa Katiba Mpya usiwe sababu ya kupigana au 
kufarakana ili kupata Katiba itakayoendelea kudumisha amani, upendo, 
utulivu na ushirikiano.
                
              
Mkapa alitoa wito huo juzi, alipokuwa akizungumza 
kwenye hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa vituo vya huduma ya 
afya mkoani hapa zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS Foundation 
kwa zaidi ya Sh1.9 bilioni.
“Vyovyote mchakato wa Katiba utakavyoishia, 
tuhakikishe tunabaki na amani na utulivu wetu kwa ajili ya ustawi wa 
nchi yetu, tuhitilafiane bila kupigana,” alisema.
Alisema Watanzania wanapaswa kwa pamoja 
wasiiharibu nchi yao na kuhakikisha kizazi cha sasa na kijacho, 
vinaendelea kuwaenzi waasisi wa Taifa kwa uadilifu mkubwa.
Akabidhi nyumba
Akikabidhi nyumba hizo, Mkapa alisema ana imani 
wananchi wanaohudumiwa na zahanati 15 zilizojengewa nyumba hizo 
wataendelea kufaidika na huduma bora kwa kuwa watumishi wameboreshewa 
mazingira ya kazi.
“Kama mnavyoona nyumba hizi ni za kisasa, zina 
maeneo muhimu yote yanayokidhi mahitaji ya binadamu, zipo imara na 
zimekidhi viwango vya ujenzi vinavyostahili,” alisema.
Aliitaka halmashauri zinazohusika kuhakikisha 
nyumba hizo zinatumika kama ilivyokusudiwa, kutunzwa vizuri na kutengewa
 bajeti ya kutosha kwa ajili ya ukarabati pale utakapohitajika ili 
ziweze kudumu kwa muda mrefu.
Vijiji vilivyonufaika vipo katika wilaya za Singida Vijijini, Iramba na Manyoni.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment