Na Nathaniel Limu, Singida
WAANDISHI wa Habari mkoani Singida, 
wamehimizwa kuondokana na uandishi habari wa mazoea na badala yake 
wabadilike na kuwa wabunifu ili kazi yao iweze kukidhi viwango vya 
wakati uliopo.
Changamoto hiyo imetolewa hivi 
karibuni na mwandishi wa habari mkongwe, Eda Sanga wakati akizungmza 
kwenye semina ya Uhabarisho wa Mfuko wa Habari Tanzania (Tanzania Media 
Fund TMF) kwa waandishi wa habari mkoa wa Singida.
Amesema waandishi wa habari ule wa business as usual, haufai umepitwa na wakati unadumaza maendeleo ya mhusika.
amesema uandishi wa habari kwa sasa 
umetakiwa mwandishi wa habari ujitume, uwe mbunifu, ufanye uchunguzi wa 
kina ili ukiandika habari watu wakupongeze au wakusifu.
  Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa 
Singida,wakifuatilia mada   zilizokuwa zinatolewa na maafisa kutoka 
Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) juu ya kuchangamkia ruzuku zinazotolewa 
na mfuko huo.Picha na Nathaniel Limu.
Kwa hali hiyo, aliwataka 
kujitathimini juu ya utendaji wao wa kila siku na wahakikishe habari zao
 zisiwe na upande moja mbali ziwe ‘balanced’.
Awali Afisa Habari wa TMF makao 
makuu,Japhet Sanga amewahimiza waandishi wa habari nchini kujenga 
utamaduni wa kuomba uwezeshaji wa fedha kutoka TMF ili pamoja na mambo 
mengine kuongeza uzoefu zaidi katika kutekeleza majukumu yao.
Akifafanua, amesema TMF inatoa ruzuku
 ya fedha kwa ajili ya waandishi wa habari kuandika habari za uchunguzi 
ambazo zinaibua mambo mengi mapya na hasa kero zinazowakabili wananchi 
wakiwemo wa vijijini.
“TMF tunaamini kwamba kwa vyo vyote 
habari za uchuguzi zitamwezesha mwandishi husika kujifunza mambo mapya 
kwa hiyo atakuwa amepanua wigo wa ufahamu wa mambo mengi”.,amesema.
0 comments:
Post a Comment