Home » » CHADEMA WAPINGA WAKE WA MARAISI KUANZISHA TAASISI

CHADEMA WAPINGA WAKE WA MARAISI KUANZISHA TAASISI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mke wa Rais Kikwete, Salma aliyeasisi Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewatuhumu Rais Jakaya Kikwete na Rais mstaafu Benjamin Mkapa kwa kugeuza Ikulu kuwa kituo cha kuanzisha taasisi binafsi.

Shutuma hizo zilitolewa juzi na Mkurungenzi wa Sera na Utafiti wa CHADEMA, Mwita Waitara, wakati akihutubia mikutano ya hadhara kwa nyakati tofauti katika kata za Saranda na Makuru wilayani Manyoni, Singida.
Waitara alisema katika uongozi wao, marais hao waliwaruhusu wake zao kuanzisha taasisi binafsi kwa kutumia rasilimali za umma.
“Rais Mkapa alimruhusu mke wake Anna, akaanzisha Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) jambo ambalo limejirudua tena kwa mke wa Rais Kikwete, Salma aliyeasisi Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA).
“Ndugu zangu, katiba iliyopo haisemi chochote kuhusu mke wa rais kutumia Ikulu kuanzisha taasisi yake,” alisema Waitara, huku akiwataka wananchi kudai katiba mpya wanayoitaka.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, rasimu ya katiba mpya iliyotolewa na Jaji mstaafu Joseph Warioba inataka zawadi zote anazopewa mke wa rais nje ya nchi, lazima iwe mali ya umma sio yake binafsi kama inavyofanyika sasa.
Mwenyekiti wa CHADEMA Singida, Shabani Limu, aliwaomba wananchi wa mkoa huo kujiandikisha kwa wingi kwenye maboresho ya daftari la wapigakura yaliyopangwa kufanyika Septemba.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa