Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Shutuma hizo zilitolewa juzi na Mkurungenzi wa Sera na Utafiti wa 
CHADEMA, Mwita Waitara, wakati akihutubia mikutano ya hadhara kwa 
nyakati tofauti katika kata za Saranda na Makuru wilayani Manyoni, 
Singida.
Waitara alisema katika uongozi wao, marais hao waliwaruhusu wake zao kuanzisha taasisi binafsi kwa kutumia rasilimali za umma.
“Rais Mkapa alimruhusu mke wake Anna, akaanzisha Mfuko wa Fursa Sawa 
kwa Wote (EOTF) jambo ambalo limejirudua tena kwa mke wa Rais Kikwete, 
Salma aliyeasisi Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA).
“Ndugu zangu, katiba iliyopo haisemi chochote kuhusu mke wa rais 
kutumia Ikulu kuanzisha taasisi yake,” alisema Waitara, huku akiwataka 
wananchi kudai katiba mpya wanayoitaka.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, rasimu ya katiba mpya iliyotolewa na 
Jaji mstaafu Joseph Warioba inataka zawadi zote anazopewa mke wa rais 
nje ya nchi, lazima iwe mali ya umma sio yake binafsi kama inavyofanyika
 sasa.
Mwenyekiti wa CHADEMA Singida, Shabani Limu, aliwaomba wananchi wa 
mkoa huo kujiandikisha kwa wingi kwenye maboresho ya daftari la 
wapigakura yaliyopangwa kufanyika Septemba.
 Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment