Kamanda
 wa jeshi la polisi mkoa wa Mbeya,Ahmed Msangi (wa tatu kulia) 
akishiriki mchakamchaka muda mfupi kabla mwenge wa uhuru kukibidhiwa kwa
 uongozi wa mkoa wa Singida, katika kijiji cha Rungwa tarafa ya Itigi 
wilaya ya Manyoni.
Na Nathaniel Limu, Singida
WAKAZI
 wa Manispaa ya Singida,wamehimizwa kulima zao la mtama linalohimili 
ukame kama inavyoelekezwa na uongozi wa mkoa ili waweze kuondokana na 
uhaba wa chakula katika kipindi chote cha mwaka.
Wito
 huo umetolewa hivi karibuni na kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 
Kitaifa,Rachael Stephen Kasanda kwa nyakati tofauti wakati akizungumza 
na wananchi wa Manispaa ya Singida katika maeneo yaliyotembelewa na 
mwenge huo.
Amesema
 zao la mtama ni zao la asili na limepewa kipao mbele na serikali ya 
mkoa kwa hivyo wakulima hawana budi kuongeza bidii katika kupanua 
mashamba ya zao hilo ili waweze kujitosheleza kwa chakula na kupata 
ziada ya kuuza wajipatie kipato.
“Kijiji
 chenu mnakiita Mtamaa,sijui linatokana na zao linalohimizwa sana na 
mkuu wa mkoa,Dk.Parseko Kone,au lina maana tofati.Lakini ukweli unabaki 
pale pale kuwa zao la mtama,ni zao pekee litakalo hakikisha mkulima 
hakabiliwi na njaa kabisa”,alifafanua.
Mkuu
 wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida,Fatuma Toufiq, (kushoto) 
akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi leo ili uweze 
kukimbizwa kwenye halmashauri ya manispaa ya Singida.
Katika
 hatua nyingine, kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa uhuru, amesema upo 
umuhimu mkubwa mtala wa elimu wa sasa ukafafanua zaidi juu ya mwenge, 
ili vizazi vya sasa na vijavyo viwe na ufahamu  mkubwa  waweze kuuenzi.
Amesema
 mtama wa sasa unataja tu uwepo wa mwenge wa uhuru bila kufafanua 
zaidi,kitendo kinachochangia kizazi cha sasa kipate wakati mgumu katika 
kujua umuhimu wake.
“Muasisi
 wa nchi hii,mwalimu Julius Nyerere,aliamua kuwasha mwenge wa uhuru muda
 mfupi baada ya Tanganyika kupata uhuru,kwa lengo kuangaza mahali hakuna
 upendo, pawepo na upendo, mahali hakuna matumaini, yawepo 
matumaini”,amesema.
Akifafanua
 zaidi amesema kwa vile mwenge wa uhuru haukutolewa ufafanuzi au kueleza
 umuhimu wake kuwepo,kunachangia baadhi ya Watanzania wachache, kuanza 
kumdhihaki  mwalimu  Nyerere bila aibu.
Baadhi
 ya wanafunzi wa shule ya msingi Ng’aida manispaa ya 
Singida,waliofanikiwa kupata nafasi adimu ya kugusa Mwenge wa uhuru 
uliozindua vyoo bora katika shule hiyo.
 “Uzoefu
 unaonyesha kuwa makundi mbalimbali ya kanda za 
wafanyakazi,yanashikamana wakati wa raha na wa taabu.Lakini nashangazwa 
na Chama cha walimu Tanzania (CWT),walimu wamekaa kimya wakati mwalimu 
mwezao hayati Julius
Nyerere,akidhihakiwa ovyo hadharani na ndani ya bunge,bila wao kutoa tamko”.amesema kiongozi huyo kwa masikitiko.
 Rachael
 amesema wakati walimu Tanzania wamekaa kimya wakati mwenzao pamoja na 
kuwa amefariki dunia miaka mingi,lakini wakiitwa kushiriki maandamano 
yasiyo na tija yo yote, haraka wanashiriki na kupoteza muda wao mwingi.
Kiongozi
 wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, Rachel Stephen Kasanda, akizindua 
rasmi choo bora cha shule ya msingi manispaa ya Singida.
Kiongozi
 wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka huu, Rachel Kasanda, 
akizungumza na wananfunzi na wazazi/walezi wa shule ya msingi Ng’aida 
manispaa ya Singida.Kulia ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Moja
 ya vyoo bora vya shule ya msingi Ngaida manispaa ya Singida 
vilivyozinduliwa jana na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, 
Rachel Kasanda ambaye alihimiza kuwepo kwa maji ya kutosha kwa ajili ya 
matumizi ya vyoo hivyo.(Picha na Nathaniel Limu).
0 comments:
Post a Comment