Home » » Wakazi wa Singida wahimizwa kulima Mtama

Wakazi wa Singida wahimizwa kulima Mtama

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

DSC08901
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mbeya,Ahmed Msangi (wa tatu kulia) akishiriki mchakamchaka muda mfupi kabla mwenge wa uhuru kukibidhiwa kwa uongozi wa mkoa wa Singida, katika kijiji cha Rungwa tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni.
Na Nathaniel Limu, Singida
WAKAZI wa Manispaa ya Singida,wamehimizwa kulima zao la mtama linalohimili ukame kama inavyoelekezwa na uongozi wa mkoa ili waweze kuondokana na uhaba wa chakula katika kipindi chote cha mwaka.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Rachael Stephen Kasanda kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Singida katika maeneo yaliyotembelewa na mwenge huo.
Amesema zao la mtama ni zao la asili na limepewa kipao mbele na serikali ya mkoa kwa hivyo wakulima hawana budi kuongeza bidii katika kupanua mashamba ya zao hilo ili waweze kujitosheleza kwa chakula na kupata ziada ya kuuza wajipatie kipato.
“Kijiji chenu mnakiita Mtamaa,sijui linatokana na zao linalohimizwa sana na mkuu wa mkoa,Dk.Parseko Kone,au lina maana tofati.Lakini ukweli unabaki pale pale kuwa zao la mtama,ni zao pekee litakalo hakikisha mkulima hakabiliwi na njaa kabisa”,alifafanua.
DSC08926
Mkuu wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida,Fatuma Toufiq, (kushoto) akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi leo ili uweze kukimbizwa kwenye halmashauri ya manispaa ya Singida.
Katika hatua nyingine, kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa uhuru, amesema upo umuhimu mkubwa mtala wa elimu wa sasa ukafafanua zaidi juu ya mwenge, ili vizazi vya sasa na vijavyo viwe na ufahamu  mkubwa  waweze kuuenzi.
Amesema mtama wa sasa unataja tu uwepo wa mwenge wa uhuru bila kufafanua zaidi,kitendo kinachochangia kizazi cha sasa kipate wakati mgumu katika kujua umuhimu wake.
“Muasisi wa nchi hii,mwalimu Julius Nyerere,aliamua kuwasha mwenge wa uhuru muda mfupi baada ya Tanganyika kupata uhuru,kwa lengo kuangaza mahali hakuna upendo, pawepo na upendo, mahali hakuna matumaini, yawepo matumaini”,amesema.
Akifafanua zaidi amesema kwa vile mwenge wa uhuru haukutolewa ufafanuzi au kueleza umuhimu wake kuwepo,kunachangia baadhi ya Watanzania wachache, kuanza kumdhihaki  mwalimu  Nyerere bila aibu.
DSC08934
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Ng’aida manispaa ya Singida,waliofanikiwa kupata nafasi adimu ya kugusa Mwenge wa uhuru uliozindua vyoo bora katika shule hiyo.
 “Uzoefu unaonyesha kuwa makundi mbalimbali ya kanda za wafanyakazi,yanashikamana wakati wa raha na wa taabu.Lakini nashangazwa na Chama cha walimu Tanzania (CWT),walimu wamekaa kimya wakati mwalimu mwezao hayati Julius
Nyerere,akidhihakiwa ovyo hadharani na ndani ya bunge,bila wao kutoa tamko”.amesema kiongozi huyo kwa masikitiko.
 Rachael amesema wakati walimu Tanzania wamekaa kimya wakati mwenzao pamoja na kuwa amefariki dunia miaka mingi,lakini wakiitwa kushiriki maandamano yasiyo na tija yo yote, haraka wanashiriki na kupoteza muda wao mwingi.
DSC08946
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, Rachel Stephen Kasanda, akizindua rasmi choo bora cha shule ya msingi manispaa ya Singida.
DSC08950
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka huu, Rachel Kasanda, akizungumza na wananfunzi na wazazi/walezi wa shule ya msingi Ng’aida manispaa ya Singida.Kulia ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
DSC08950 DSC08941
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Ngaida manispaa ya Singida vilivyozinduliwa jana na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Rachel Kasanda ambaye alihimiza kuwepo kwa maji ya kutosha kwa ajili ya matumizi ya vyoo hivyo.(Picha na Nathaniel Limu).

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa