Kaimu
 mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Singida, Joseph Sabore 
(anayeangalia kamera) akizungumza na maafisa wa shirika lisilo la 
kiserikali la Health Actions Promotion Association (HAPA), YMC na 
WaterAid Tanzania, ambao wako katika halmashauri hiyo kufanya tathimini 
ya mradi wa ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia. 
Mradi huo unaotarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi 1.6 bilioni, 
unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu na unatarajiwa kufikia 
ukingoni Desemba mwaka huu.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida 
MRADI
 wa ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia (TMEP) 
unaotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya ya Singida,umeanza kuzaa 
matunda yanayotarajiwa baada ya asilimia 89 ya wanaume kubadilika na 
kuanza kusindikiza wake zao kliniki na vituo vya afya.
Hayo
 yamesemwa hivi karibuni na Muuguzi Mkuu wa Halmashauri hiyo,Bertha 
Herman wakati akitoa taarifa yake ya ushiriki sawa wa wanaume katika 
afya ya uzazi na ujinsia, kwa maafisa wa shirika lisilo la kiserikali la
 Health Actions Promotion Association (HAPA),YMC na WaterAid 
Tanzania,ambao wanafanya tathimini ya mradi huo wa miaka mitatu 
unaotarajiwa kumalizika desemba mwaka huu.
Amesema
 katika miaka ya nyuma ambayo ilikuwa imetawaliwa na mfumo kandamizi 
(mfumo dume),ilikuwa mwiko kwa mwanaume kumsindikiza mke wake kliniki au
 kumsaidia kazi za nyumbani ikiwemo ya kufua nguo za watoto,kuandaa 
chakula na kusafisha mazingira ya kaya yao.
Amesema
 mfumo huo kwa kiasi kikubwa ulipunguza mawasiliano baina ya mke na mume
 na ulijenga utamaduni wa kuwa mwanaume ana haki ya kumpa kipigo kikali 
mke pindi anapoona inafaa.
“Baada
 ya kuanzishwa kwa mradi huu miaka mitatu iliyopita,mambo yanaendelea 
kubadilika kwa kasi kubwa.Kwa sasa si rahisi kusikia mwanaume amempiga 
mke wake.
“Wanaume
 wametambua kuwa wana wajibu wa kusindikiza wake zao kliniki kwa faida 
kwamba wanaweza kujua mapema kama kuna tatizo.Pia wanaume wengi sasa 
wanawapeleka watoto wao wachanga kliniki,kuwaogesha na kufua nguo 
zao.Kwa ujumla mradi huu umeboresha mno ndoa za wanafamilia 
wengi”,alifafanua.
Kwa
 upande wake mkazi wa kijiji cha Mtamaa Manispaa ya Singida,Mohammed 
Alute amesema elimu waliyoipata kupitia mradi wa TMEP, imesaidia mno 
wanandoa kushirikiana katika kutekeleza majukumu yote ya kifamilia 
ambayo hapo zamani,aliachiwa mwanamke peke na kuchangia kudhoofisha afya
 za akina mama.
“Kwa
 upande wangu na kwa kweli kwa wanaume wengi waliopata elimu inayotolewa
 na mradi wa TMEP,hatuoni kinyaa kupika chakula,kwenda kiliniki au kufua
 nguo za familia.Kumbe mwanamke akisaidiwa kazi za nyumbani,hachakai 
wale hazeeki upesi na kwa ujumla ushiriki huu,unaongeza mapenzi zaidi 
baina ya wana ndoa”,amesema Alute.
Naye
 Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Singida,Joseph Sabore 
amesema mradi wa TMEP,umeleta mabadiliko makubwa kwa wakazi wa 
halmashauri hiyo ambapo sasa wanandoa wanaweza kukaa pamoja na kupanga 
utaratibu wa uzazi wa mpango kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Amesema
 wamejiandaa vema ili kuendeleza mradi huo wakati TMEP itakapoacha 
kusimamia utekelezaji wa mradi huo.Elimu na uhamasishaji utaendelezwa 
kwa jamii na katika shule za msingi,sekondari na vyuo.
Mradi huo unaotarajiwa kumalizika desemba mwaka huu,unatekelezwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi 1.6 bilioni.
0 comments:
Post a Comment