Mratiibu
 msaidizi wa polisi mkoa wa Singida,Irene Mbwatila,(anayeangalia 
kamera),akizungumza na timu ya pamoja ya maafisa wa shirika la HAPA,YMC 
na RFSU, inayofanya utafiti juu ya mradi wa ushiriki sawa wa wanaume 
katika afya ya uzazi na ujinsia.
Baadhi
 ya wanaume wakiwa na wake zao wakazi wa kijiji cha Ntuntu wilaya ya 
Ikungi mkoa wa Singida, wakiwa kwenye foleni katika kliniki ya kijijini 
hapo,wakisubiri kuingia kumwona muuguzi. Elimu iliyotolewa kwa pamoja na
 mashirika ya HAPA na YMC,ya umuhimu wa ushiriki sawa wa wanaume katika 
afya ya uzazi na unjisia, katika kipindi cha miaka mitatu, imechangia 
wanaume pamoja na mambo mengine, kusindikiza wake zao kliniki kutoka 
asilimia 0 hadi 80 ya sasa.
Muuguzi
 wa zahanati ya kijiji cha Ntuntu wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Mary
 Lema, akitoa dawa kwa mama mjamzito Lucia Hongoa, huku mume wake Edward
 akiwa anashuhudia. Kijiji cha Ntuntu ni moja ya vijiji ambavyo elimu ya
 ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia,inatolewa.
Muuguzi
 wa zahanati ya kijiji cha Ntuntu wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Mary
 Lema akitoa taarifa yake juu ya utekelezaji wa mradi wa ushiriki sawa 
wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia kwa waandishi wa habari 
(hawapo pichani). (Picha na Nathaniel Limu). 
Na Nathaniel Limu, Ikungi
 ELIMU
 ya ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia inayotolewa
 kwa pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali ya HAPA na YMC imezaa 
matunda baada ya wanaume kubadilika, na kuanza kusindikiza wake zao 
klinki na kusaidia kazi zote za nyumbani,imeelezwa.
Akizungumza
 na waandishi wa habari ofisini kwake, muuguzi wa kliniki ya zahanati ya
 kijiji cha Ntuntu wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Mary Lema, amesema 
kuwa miaka mitatu iliyopita,hakukuwa na mwanaume anayesindikiza mke wake
 klinki.
Alisema
 elimu hiyo imewahamasisha na kuwaelimisha wanaume ambao kwa sasa 
wanashiriki kikamilifu, afya ya uzazi na ujinsia kutoka asilimia 0 hadi 
80.
Lema amesema kuwa kwa sasa kama mwanaume hajamsindikiza mke wake mjamzito kliniki,atafanya hivyo kwa sababu za msingi.
“Kwa
 kawaida wanaume wakazi wa wilaya hii na mkoa kwa ujumla,huwa ni mwiko 
kusindikiza mke kliniki au kufanya kazi zingine za nyumbani kama kufua 
nguo,kupika,kuchota maji na kusenya kuni.Lakini baada ya elimu hii ya 
ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na ujinsia 
kutolewa,wanaume karibu wote,wamebadilika”,alifafanua.
Akifafanua
 zaidi,alisema kuwa wanaume karibu wote wa kijiji cha Ntuntu kwa sasa 
wanafanya/wanashiriki  shughuli zote za nyumbani sawia na 
wanawake,kitendo kinachoboresha sana mahusiano na mapenzi.
Kwa
 upande wake Ana Charles, amesema kuwa baada ya elimu hiyo kutolewa 
kijijini hapo, wanaume wamebadilika mno kwa kuwa wapole, kuwahi kurudi 
nyumbani na mapenzi yameboreka zaidi.
“Kwa
 sasa wanaume wetu wamejenga tabia ya kuambatana nasi kwenda kupata moja
 baridi kitendo ambacho hakikuwepo miaka mitatu iliyopita.Pia wamekuwa 
wapole hatupigwi ovyo kama ilivyokuwa zamani”,amesema Ana huku 
akitambasamu.
0 comments:
Post a Comment