Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Hayo yamesemwa na Meneja wa shirika hilo lisilo la kiserikali, Ivo 
Manyaku mkoani hapa mwishoni mwa wiki, alipotoa taarifa ya utekelezaji 
wa programu hiyo.
Manyaku alitaja vifaa vilivyonunuliwa kwa lengo la kuwasaidia 
wakulima kuwa ni vinyago 30, fremu 48 zenye ujumbe mbalimbali, shajara 
33, mabango 48, vipeperushi 300 na magari sita ya abiria yamebandikwa 
stika zenye ujumbe.
“Lengo kuu la hii programu ni kuona wadau mbalimbali wakiwemo 
serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi na raia mwenyewe 
wakishirikiana, wakiwajibika na kuchukua hatua kukabiliana na mabadiliko
 ya tabia nchi ngazi zote,” alisema.
Alisema madhara yanayosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi ni joto,
 ukame, mafuriko, vimbunga vikubwa, magonjwa na kupungua kwa vina vya 
maji katika vyanzo mbalimbali.
Alisema upo uwezekano wa kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya 
tabia nchi kwa wakulima ikiwa ni pamoja na  kuendesha kilimo  bora na 
ufugaji wenye tija.
 Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment