Home » » SEMA YATUMIA MIL.25/-KUSAIDIA WAKULIMA

SEMA YATUMIA MIL.25/-KUSAIDIA WAKULIMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Meneja wa SEMA, Ivo ManyakuSHIRIKA la Mpango  Endelevu wa Uboreshaji Mazingira (SEMA), limetumia zaidi ya sh milioni 25 kununua vifaa vyenye ujumbe utakaowasaidia wakulima kubadilika ili kuendana na mabadiliko ya tabia nchi.

Hayo yamesemwa na Meneja wa shirika hilo lisilo la kiserikali, Ivo Manyaku mkoani hapa mwishoni mwa wiki, alipotoa taarifa ya utekelezaji wa programu hiyo.
Manyaku alitaja vifaa vilivyonunuliwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima kuwa ni vinyago 30, fremu 48 zenye ujumbe mbalimbali, shajara 33, mabango 48, vipeperushi 300 na magari sita ya abiria yamebandikwa stika zenye ujumbe.
“Lengo kuu la hii programu ni kuona wadau mbalimbali wakiwemo serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi na raia mwenyewe wakishirikiana, wakiwajibika na kuchukua hatua kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ngazi zote,” alisema.
Alisema madhara yanayosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi ni joto, ukame, mafuriko, vimbunga vikubwa, magonjwa na kupungua kwa vina vya maji katika vyanzo mbalimbali.
Alisema upo uwezekano wa kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi kwa wakulima ikiwa ni pamoja na  kuendesha kilimo  bora na ufugaji wenye tija.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa