Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
BARAZA Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Singida limemsimamisha
 uongozi Mwenyekiti wao wa mkoa, Martin Labia Lissu kwa madai ya 
kushindwa kutoa utetezi dhidi ya tuhuma zilizokuwa zikimkabili.
Katika kikao chake kilichofanyika jana kwenye ofisi za CCM Mkoa wa 
Singida na kuhudhuriwa na wajumbe 24 wa baraza hilo kwa kauli moja 
wameridhia hatua hiyo na kutoa mapendekezo kwa mamlaka husika kwa hatua 
zaidi.
Mwenyekiti wa kikao hicho, Joseph Saenda aliwaambia waandishi wa 
habari kuwa kikao kilikuwa na agenda moja ya kumwita mbele ya baraza 
mwenyekiti wao, Lissu.
Alisema baraza baada ya kujadiliana kwa pamoja, wajumbe 
hawakuridhishwa na majibu ya utetezi wake, kwani hakuonesha kukiri 
kufanya makosa mbele ya wajumbe wa kikao.
“Baada ya mjadala wa muda mrefu baraza limemsimamisha uongozi, kwa 
mujibu ya katiba ya UVCCM ibara ya 78 (i) na kutoa mapendekezo ya kumvua
 uongozi kwa ngazi ya juu yenye mamlaka hayo kikatiba,” alisistiza.
Mei 17 mwaka huu, wajumbe wa baraza hilo kwa kauli moja walidai 
kutokuwa na imani na uongozi wa mwenyekiti huyo kutokana na kutumia 
vibaya madaraka yake na kuwa mtovu wa nidhamu na kudharau viongozi wa 
juu wa chama.
Saenda aliorodhesha tuhuma zilizokuwa zikimkabili Mwenyekiti huyo 
kuwa ni kushindwa kuitisha vikao tangu achaguliwe mwaka 2012 na 
kushindwa kushiriki ziara mbalimbali za viongozi ndani ya chama. 
Mwenyekiti huyo pia alikuwa akituhumiwa kuwa mchonganishi kati ya 
viongozi wa UVCCM na chama na kushindwa kufanya kazi zake na badala yake
 kujikita zaidi kwenye kampeni za mmoja wa wagombea nafasi ya urais 
mwakani. 
Meneja wa duka jipya la huduma kwa wateja la Vodacom lililopo Sinza 
Afrika Sana jijini Dar es Salaam, Swaum Manengelo akifungua mlango 
kuashiria ufunguzi rasmi wa duka hilo uliofanyika juzi.
Chanzo:Tanzania Daima  
0 comments:
Post a Comment