Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ZAIDI ya abiria 700  waliokuwa wakisafiri na treni ya abiria 
wakitokea Kigoma kuelekea Dar es  Salaam, wamekwama kwa siku mbili 
wilayani Manyoni, baada ya treni ya mizigo  kuanguka.
  Wakizungumza na  waandishi wa habari waliofika eneo hilo  jana, abiria
 hao wamelilalamikia Shirika la Reli kutokana na kutokuwa na  utaratibu 
mzuri wa kusafirisha abiria wake pindi tatizo linapojitokeza.
  Walisema walipofika  Manyoni majira ya mchana, walielezwa kuwa treni 
ya mizigo ilikuwa imeanguka  kituo kinachofuatia cha Saranda, hivyo 
wasubiri utaratibu.
  “Lakini cha kushangaza mabasi ambayo yalikuwa  yakiletwa na Shirika la
 TRL yalikuwa machache kwa sababu abiria tulikuwa  wengi,” alisema mmoja
 wa abiria hao, Anton Beni.
  Walisema kutokana na  hali hiyo walilazimika kulala nje huku wakiwa na
 watoto wadogo na wengine  wagonjwa, kwani mabasi yalipokuwa yakifika 
kuwachukua hakukuwa na utaratibu na  kusababisha watu kugombea na kusema
 hadi sasa baadhi ya abiria hawajui hatima yao ya kufika Dar es  Salaam.
  Meneja wa Kanda wa TRL  kutoka Dar es Salaam,  Philipo Rutizibwa, 
alisema suala la abiria waliokwama Manyoni wameshafanya  utarabu wa 
mabasi na yameshaanza kuwachukua kuwapeleka wanakokwenda
 Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment